Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Zari Hassan akana madai ya kuomba shabiki pesa na kukataa kuziregesha

F9283399fbb44c37 Zari Hassan akana madai ya kuomba shabiki pesa na kukataa kuziregesha

Wed, 9 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Zari Hassan amekanusha madai kwamba alikopa pesa na kukataa kuzirejesha

- Kulingana na Zari, alipewa barua ya kudai kwamba alipe KSh 93,000 anayodaiwa kukopa

- Walakini, Zari alimfokea mlalamishi akisema wanalaumiwa kwa kutokuwa waangalifu

Zari Hassan amejitenga na jamaa mmoja ambaye amedai alimtapeli pesa mmoja wa mashabiki wake

Kupitia mtandao wa Instagram, sosholaiti huyo ambaye pia ni mfanyabiashara anayeishi Afrika Kusini aliwaonya mashabiki kwamba hausiki kivyovyote na hatochukua jukumu la watu wasio waaminifu wanaojifanya kuwa yeye.

Kulingana na Zari, jamaa huyo aliyejifanya kuwa yeye (Zari) alidaiwa kukopa pesa kutoka kwa mmoja wa mashabiki wake na akashindwa kuirejesha.

Alipakia barua ya kudai ambayo alikuwa amepokea akiombwa alipe KSh 93,000, na ikiwa angekosa mlalamishi angemburuta kortini.

Zari alijibu vikali barua hiyo.

“Nitaendelea kukuonya, ibiwa kwa sababu ya akili zako ndogo. Hauwezi kutumia pesa watu usiowajua, na nisikuite mjinga. Wewe ni mjinga aliyethibitishwa,” aliandika.

Mama wa watoto watano zaidi alisema atawafichua wale wanaochafua jina lake zuri huku akisema kwamba hajawahi kuomba msaada wa kifedha.

Mwanamuziki huyo wa zamani alisema zaidi kwamba hapeleki watu nje ya nchi kufanya kazi.

"Sijawahi kuomba msaada wa kifedha kutoka kwa mtu yeyote, sikuwahi kutangaza kazi nje ya nchi, sitafuti pesa za hisani. Mimi peke yangu hufanya misaada yangu. Tafadhali usiniletee upuuzi wako,” Zari alisema.

Aliwaambia wahasiriwa waacha kuacha kumsumbua wakati akiuliza ni vipi wanaweza kudanganywa kwa urahisi mkondoni, lakini mtu anaweza kupata chuo chake kwa urahisi Afrika Kusini kwenye Ramani za Google.

“Hatimaye alikwenda kwenye ukurasa wangu halisi na kupata barua pepe yangu halisi. Swali ni kwamba, kwanini hakutumia njia ile ile kuniuliza ikiwa watu ambao alikuwa akiongea nao ni halali? Kwa nini sasa?” Zari aliuliza.

KSh 93,000 ni kama tone la bahari kwa Zari, kutokana na utajiri wake.

TUKO.co.ke iliripoti kuwa Zari ana mkusanyiko wa magari yenye thamani ya zaidi ya KSh 30 milioni.

Karakana ya Mkurugenzi Mtendaji wa Chuo cha Brooklyn City ina Ranger Rover, Mercedes Benzes na Chrysler.

Gari la gharama kubwa zaidi linalomilikiwa na Zari ni Bentley ambayo Diamond Platnumz alimsaidia kununua.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke