Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Willy Paul afichua sababu iliyomfanya aache kufanya miziki za Injili

0fgjhs6cbgvpuhi6t Willy Paul afichua sababu iliyomfanya aache kufanya miziki za Injili

Thu, 10 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Willy Paul amefichua sababu iliyomfanya aache kuimba nyimbo za injili

- Kulingana na Willy baadhi ya wasanii wenzake wakiwemo maDJ walikuwa wakimnyanyasa na kumpiga vita katika ulingo wa sekta ya injili

- Willy pia alifichua kuna wakati alikumbwa na msongo wa mawazo kwa zaidi ya miezi minne, hangeweza kumudu kulipa bili licha ya nyimbo zake kuvuma na kufanya vema nchini

- Mashabiki wake wamemshauri asitikisike wala kujali yale yanayosemwa na maadui wake

Mwanamuziki maarufu Willy Paul amevunja kimya chake kuhusu sababu iliyomfanya aache kufanya muziki wa injili licha ya nyimbo zake kuvuma na kupendwa na mashabiki.

Willy alifichua kwamba kuna watu wenye roho chafu katika sekta ya injili ambao walimnyanyasa na kufanya afilisike kiwango cha yeye kushindwa kulipa bili zake.

" Umewahijiuliza ni kwa nini watu wanaweza kuchukia bila sababu? kuna maadui, wanatamani wangelikuwa na kile ulichonacho, wanatamani wangelikuwa wewe hata kwa robo ya sehemu yako,"

" Ni kipi sijakiona kwa hii maisha? maisha ya ufukara, maisha matamu na ya kupendeza, wanawake warembo nakadhalika. Watu wamenichukia bila sababu lakini sijakata tamaa, nitaendelea kukuwa mimi," Alisema Willy.

Kulingana na Willy, watu waliokuwa wakimpiga vita katika sekta ya injili ndio waliokuwa mstari wa mbele kumuuliza sababu ya yeye kuondoka katika sekta hiyo.

" Chuki kutoka kwa wanamuziki wenzangu na maDJ, kukosa kucheza miziki zangu na mapendeleo ilifanya niamue kuchukua njia mbadala. Najua nilikuwa staa lakini watu wenye roho chafu hawangefurahia kuniona niking'aa. Hawa watu walinivunja moyo sana, walinifanya niwe na msongo wa mawazo kwa zaidi ya miezi minee." Aliongezea Willy.



Hata hivyo, baadhi ya mashabiki wake wamemshauri asikate tamaa wala asitikisike na yale maadui wake wanayosema kumhusu.

Kama ilivyoripotiwa awali na TUKO.co.ke, mwanamuziki Ringtone aliwakashifu Wakenya wengi haswa wakristo kwa kutowasaidia na kuunga mkono wasanii wanaofanya miziki za injili.

Madai hayo yaliibui hisia mseto miongoni mwa wanamitandao ambao baadhi walidai kwamba muziki za Kenya huwa hazina maudui.

Read: ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke