Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya "wapandisha" bei ya mafuta nchini Tanzania

Mafuta Wakenya

Tue, 21 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Madereva Wakenya ambao wamekuwa wakikimbia taifa jirani la Tanzania kununua mafuta, wamesababisha bei ya petroli kupandishwa nchini humo kutokana na kuongezeka kwa mahitaji.

Bei ya petroli imepandishwa nchini Tanzania kutokana na kuongezeka kwa mahitajiVituo vya kuuza mafuta ya petroli Tanzania sasa vinauza lita moja ya petroli kwa KSh 137.15 kutoka 98.30 kufuatia kufurika kwa wateja kutoka Kenya.

Madereva hao walikuwa wa kutoka kaunti za Kisii, Homa Bay na Migori.

Vituo vya kuuza mafuta ya petroli nchini Tanzania sasa vinauza lita moja ya petroli kwa KSh 137.15 kutoka 98.30 kufuatia kufurika kwa wateja wengi kutoka Kenya.

Kwa mujibu wa Taifa Leo, madereva hao walikuwa wa kutoka kaunti za Kisii, Homa Bay na Migori.

Serikali ya Kenya yapandisha bei ya mafuta maradufuMnamo Jumatano, Septemba 15, serikali kupitia Mamlaka ya Kawi na Petroli nchini (EPRA), iliongeza bei ya mafuta ya petroli kwa KSh 7.58, kila lita ikiuza KSh136.30 huku mafuta ya dizeli na ya taa yakipanda kwa KSh7.94 na KSh12.97.

Kufuatia ongezeko hilo, Wakenya wamekuwa wakivuka mipaka na kuingia mataifa jirani ya Uganda na Tanzania kununua mafuta ya bei nafuu.

Viongozi wateta kuhusu kuongezeka kwa bei ya mafutaKutokana na nyongeza hiyo bei ya mafuta, Wakenya wengi walikerwa wakiwemo viongozi.

Wakiongozwa na kiongozi wa chama cha Wiper, Kalonzo Musyoka, viongozi hao waliishutumu serikali vikali kwa kuongeza bei za mafuta wakidai ni mzigo kwa mwananchi wa kawaida.

Kulingana na Musyoka, kuongezeka kwa bei ya mafuta, kutafanya nchi kushindwa kukabiliana na umaskini.

Kwa upande wake kinara wa Upinzani, Raila Odinga, alibainisha kuwa ongezeko la gharama ya mafuta ni pigo kwa Wakenya ambao wanazama katika deni kutokana na athari za COVID-19.

Alilaani serikali kwa hatua hiyo akitoa wito kwa hatua za haraka kuchukuliwa ili kuwaokoa Wakenya na mzigo mzito wa kudora kwa uchumi.

Naibu Rais William Ruto pia aliwataka washikadau katika sekta hiyo kuandaa mkutano na wabunge ili kupata suluhu la kudumu kuhusu ongezeko hilo.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke