Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya walalamika gharama ya maisha baada ya bei za bidhaa kupanda

Ebdfc94d137661fd Wakenya walalamika gharama ya maisha baada ya bei za bidhaa kupanda

Tue, 16 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Bei za bidhaa muhimu kama vile mkate na sukari zimepanda huku msimu wa sikukuu ukikaribiaKula kiamsha kinywa itakuwa ni gharama baada ya bei ya mkate wa gramu 400 kuongezeka kwa shilingi 5, huku bei ya maziwa ikipanda kwa shilingi 5 Watengenezaji mafuta ya kupikia pia wamepandisha bei kutoka shilingi 250 kwa lita hadi shilingi 300 Wakenya watalazimika kujikaza kisabuni kwa kugharamika zaidi ili kununua mkate, soda, sukari na mafuta ya kupikia, huku msimu wa sikukuu ukikaribia.

Hii ni baada ya watengenezaji kuongeza bei za bidhaa, kwa kile kinachoonekana kuchochea mfumko wa bei.

Kulingana na ripoti iliyochapishwa na jarida la Business Daily, gharama ya kiamsha kinywa imeathirika pakubwa baada ya bei ya mkate wa gramu 400 kuongezwa kwa shilingi 5, huku bei ya ngano ikizidi kupanda katika masoko ya kimataifa.

Wakati huo huo, bei ya kilo moja ya sukari iliuzwa kwa shilingi 130 kwa kilo mwezi mmoja uliopita, sasa itauzwa kwa shilingi 140.

Wakati huohuo mililita (ml) 200 ya soda imeongezwa kwa shilingi 5 na sasa itauzwa kwa shilingi 25, huku mililita 300 ya soda ikiongezeka kwa shilingi 5 na kuuzwa kwa shilingi 35.

Watengenezaji wa mafuta ya kupikia vilevile wameongeza bei kutoka shilingi 250 kwa lita hadi shilingi 300.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke