Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Wakenya Wamuomboleza Mwanariadha Bingwa Agnes Tirop Kufuatia Kifo cha Ghafla

A11fad19c63602a6 Wakenya Wamuomboleza Mwanariadha Bingwa Agnes Tirop Kufuatia Kifo cha Ghafla

Thu, 14 Oct 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mwanariadha bingwa Agnes Tirop alipatikana akiwa ameuawa ndani ya nyumba yake eneo la Iten Jumatano, Oktoba 13 Mwili wake ulipatikana na majeraha kwenye tumbo, ishara kwamba huenda mwathiriwa aliuawa kwa kudunga kisuWakenya mitandaoni akiwemo Rais Uhuru Kenyatta wameomboleza kifo cha mwanariadha huyoAgnes Tirop ambaye alikuwa bingwa wa mbio za mita 5,000 katika Olimpiki za Tokyo za 2020 alipatikana akiwa ameuawa nyumbani kwake huko Iten, kaunti ya Elgeyo Marakwet Jumatano, Oktoba 13.

Mwili wa mwendazake Agnes ulipatikana ndani ya nyumba yake eneo la Iten kaunti ya Elgeyo Marakwet ukiwa na majeraha kwenye tumbo.

Wakenya kupitia mitandao ya kijamii wameomboleza kifi cha mwanariadha huyo ambaye nyota yake ilikuwa imeanza kunga'a.

TUKO.co.ke iliweza kukusanya baadhi ya jumbe ambazo Wakenya wametumia familia kupitia mitandao ya kijamii

" Nimehuzunishwa na kifo cha Agnes Tirop, bingwa wa kimataifa wa mbio za mita 5,000 katika Olimpiki Tokyo za 2020, aliuawa kinyama nyumbani kwake eneo la Iten, natumai polisi watafanya uchunguzi wa kina kuwakamata washukiwa," Seneta wa Elgeyo Marakwet Kipchumba Muromen aliandika.

"Tumeshtuka kufuatia kifo cha bingwa wetu wa kimataifa wa riadha Agens Tirop, alikuwa mwanariadha ambaye nchi ilikuwa inatazamia kwa ushindi mkubwa zaidi," Chama cha Wanariadha nchinikiliandika.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke