Wed, 22 May 2024
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Kenya, Dk. William Ruto, ametangaza kuwa Wakenya 5,000 wataanza kufanya kazi na kampuni za Marekani kupitia kampuni iliyopo Ruiru.
Akiwa nchini Marekani, Rais Ruto amesema, Kampuni hii inatarajia kuajiri Wakenya 5,000 kwa kazi za mtandaoni, ambapo watafanya kazi wakiwa Ruiru lakini kwa kampuni za Marekani.
"Teknolojia ya kidijitali itasaidia Wakenya kufanya kazi kutoka Ruiru kwa kampuni za Marekani" Rais Ruto alisisitiza nakuongeza kuwa katika kipindi cha miaka miwili ajira hizo zinatarajiwa kufikia zaidi ya wakenya 20,000.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live