Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Shaffie Weru amzawadi bintiye gari aina ya Jeep

979b0cc46042043f Shaffie Weru amzawadi bintiye gari aina ya Jeep

Sat, 26 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Aliyekuwa mtangazaji wa stesheni ya redio ya Kiss 100 Shaffie Weru anajivunia kuwa baba wa msichana wa miaka 16.

Kupitia mtandao wa Instagram Shaffie aliposti picha ya binti wake Milan akiwa ndani ya gari aina ya Jeep ambalo alimzawadi siku yake ya kuzaliwa.

Shaffie alimtakia heri njema bintiye anaposherehekea miaka 16," Happy Birthday Milenree," Shaffie aliandika akiwa mwingi wa furaha.

Haijabainika iwapo Shaffie alinunua gari hilo pekee au alisaidiana na mamake Milan, Debbie Asila ambaye anaishi naye nchini Marekani.

Ni siku tatu zimepita baada ya Shaffie pia kumtakia bintiye kila la heri na maisha marefu.

" Mwaka wa 2005 nilibarikiwa na mtoto wangu wa kwanza, wakati huo ndio niliweka tatoo kwa mkono wangu kusherehekea ujio wake duniani. Kwa siku tatu zijazo atakuwa anatimia umri wa miaka 16 Allahamdulillah," Shaffie alisema.

" Nilikuwa baba kama sijamea ndevu, kabla ya enzi za tatoo na kabla niwe super star na sasa niko rockstar hivyo ndivyo wenzangu wanavyoniita," Aliongezea Shaffie.

TUKO.co.ke inafahamu kwamba Shaffie amekuwa akisafiri mara kwa mara kwenda Marekani kumtembelea bintiye. Wawili hao wana uhusiano wa dhati kulingana na picha ambazo mtangazaji huyo hupakia mitandao wakiwa pamoja.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke