Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rapa King Kaka na mkewe Nana Owiti waadhimisha miaka kumi ya ndoa

D7338224f2c91f78 Rapa King Kaka na mkewe Nana Owiti waadhimisha miaka kumi ya ndoa

Mon, 24 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rapa King Kaka na mkewe Nana Owiti wameadhimisha miaka 10 katik ndoa yao

- Wanandoa hao walifuchua kwamba huwa wanaiga mfano wa ndoa ya wanamuziki Nameless na Wafu ambao wamekuwa katika ndoa kwa miaka 15

- King Kaka na Nana kwa pamoja wamejaliwa watoto wawili, wa kike na wa kiume

Staa wa rap Kennedy Ombima maarufu King Kaka na mkewe Nana Owiti waliadhimisha miaka 10 ya kuwa katika ndoa Jumapili, Mei 25.

Kwenye ujumbe wake aliouposti kwenye mtandao wa Instagram, King Kaka alisema kama ndoa zingine zile, yao pia imekumbwa na changamoto nyingi lakini anashukuru Mungu mahali wamefika.

King Kaka aliandika," Leo inatimia miaka 10 ya penzi langu na rafiki yangu Nana Owiti. Tumepitia panda shuka nyingi, tumetofautiana, tumeelewana lakini mwishowe ni sisi tu. Mungu ametuongoza katika kila hali, namshukuru Mungu kwa kunipa mke mrembo mwenye roho safi.Asante kwa kusimama nami, asante kwa familia ya kupendeza. Asante kwa kunipenda na nakuahidi mimi na wewe hadi tukunje mgongo."

Kwa upande wake Nana alifichua kwamba yeye huiga mfano wa ndoa ya wanamuziki Nameless na Wahu ambao wamekuwa katika ndoa kwa miaka 15 sasa.

" Miaka 10 tukiwa pamoja, Babe mimi ni wako milele, hakuna marejesho,Nakupenda sana" Nana aliandika.

Msanii huyo huanika wazi penzi lake mitandaoni na hivi punde alimbikizia sifu mkewe siku yake ya kuzali, alidai amekuwa nguzo kwa ndoa yao, bila yeye haingekuwa imenawiri.

King Kaka alimshuku Mungu kwa mke mrembo, mwenye roho safi na ambaye anatamani na kila mtu.

" Mali safi, asante kwa kusimama nami katika kila hali, nilipokuwa sina chochote hadi kwa sasa, Asante kwa kuwa nguzo kwa ndoa yetu, asante kwa kushikilia ubavu wangu," King Kaka alisema akimtakia heri njema siku ya kuzaliwa.

Wanandoa hao kwa pamoja wamejaliwa watoto wawili, wangelikuwa na watatu lakini walimpoteza mmoja baada ya mimba ya Nana kutoka miaka kadhaa iliyopita.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke