Rapa maarufu Khaligraph Jones amefichua kwamba mamake ni mhubiri na amekuwa akimuombea afanikiwe katika taaluma yake ya muzikiKulingana na Khaligraph, alilelewa katika familia ya kumcha Mungu na anaamini ndio sababu amefanikiwa maishaniAidha, babake Khaligraph alifariki dunia mwaka wa 2002 kabla kushuhudia mafanikio ya mwanaweRapa maarufu Brian Ouko Omollo maarufu Khaligraph Jones amefichua mambo machache kuhusu familia yake.
Akiwa kwenye mahojiano na mwanahabari wa Radio Jambo Massawe Japanni, Khaligraph alifichua kwamba mamake ni mhubiri na amekuwa akimuomba kila siku ili afanikiwe katika taaluma yake ya muziki.
Khalighraph ambaye ni baba wa watoto watatu alifichua kwamba alilelewa katika familia ya kikristo na mama yao angewaombea kila usiku kabla walale.
" Ulilelewa katika kanisa? Mwanahabari Massawe aliuliza
" Ndio tena kabisa, mamangu alikuwa mhubiri, hata tunavyozungumza kwa sasa bado anachapa injili," Khaligraph alisema.
Kulingana na Khaligraph, angependa sana babake aone jinsi amefanikiwa maishani lakini alifariki dunia mwaka wa 2002 kama bado anang'ang'ana kimziki.
Kwenye video ambayo imesambaa kwa sasa mitandaoni, Khaligraph alikuwa anamshukuru mamake kwa kumuombea kila mara ili aweze kufanikiwa maisha.
" Mamangu alipitia katika studio zetu kupata nakala ya album yangu ya 1990 na aliamua atuombee kwanza, anataka album hii ipate soko," Khaligraph alisema.
" Ni kwa ajili ya uvumilivu tu, Mungu ametundea makuu, tunamshukuru na kumpa sifa. Asante sana kwa yote," Alisema Mamake Khalighraph.
Msanii huyo pia alifichua kwamba babake aliaga dunia mwaka wa 2002 kabla hajashuhudia mafanikio yake, angepende awe hai amuone mwanawe jinsi alivyo staa.
Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Tazama habari za TUKO hapa