Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Uhuru atangaza Kenya itandelea kuandaa Mbio za Magari Duniani hadi 2026

94bb6a671b985d70 Rais Uhuru atangaza Kenya itandelea kuandaa Mbio za Magari Duniani hadi 2026

Mon, 28 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Huku Mbio za Magari Duniani (WRC) Safari Rally zilipofunga jamvi, Rais Kenyatta alitangaza kuwa mashindano hayo yataendeleaHii ni baada ya kutangaza kuwa Kenya itaendelea kuwa mwenyeji wa mashindano hayo kila mwaka hadi 2026 Kenyatta alisema serikali imekubaliana na Mbio za Magari Duniani (WRC) na Shirikisho la Mbio za Magari Duniani (FIA)

Huku Mbio za Magari Duniani (WRC) Safari Rally zilipofunga jamvi Jumapili, Juni 27, Rais Uhuru Kenyatta alikuwa na habari njema kwa Wakenya.

Akihutubia umma kabla ya washindi kutangazwa, Uhuru alitangaza kuwa Kenya imeingia katika makubaliano na Mbio za Magari Duniani (WRC) na Shirikisho la Mbio za Magari Duniani (FIA) kuandaa mashindano hayo kila mwaka hadi 2026.

Uhuru aliwasili Hells Gate WRC Circuit mjini Naivasha kushuhudia fainali ya makala ya 2021 ya Safari Rally akiwa ameandamana pamoja na Waziri wa Michezo Amina Mohammed.

Mashindano hayo ambayo yaliandaliwa kati ya Juni 24 na 27, yamekadiriwa kuwa nzito zaidi duniani.

Tangazo hilo la Kenya kuwa mwenyeji ni baada ya miaka 19, huku kurejea kwa hafla hiyo kubwa ikitoa nafasi ya taifa kuanika urembo wake na kupiga jeki uchumi.

Hii ni moja ya ufanisi wa Rais Kenyatta katika kutimiza hadi zake tangu achukuwe hatamu za uongozi miaka minane iliyopita.

Tangazo la Uhuru lilipokelewa vyema na Wakenya

@Dennis_Kyallo1: "Makubaliano ya kuwa mwenyeji wa #SafariRallyKenya hadi 2026 inakaribishwa"

@jasonlongmen: "Hakuna tena liizo za kigeni. Nitakuwa ninasubiri WRC kila mwaka hadi 2026."

Mfaransa Sebastien Ogier ndiye mshindi wa Mbio za Magari Duniani (WRC) Safari Rally makala ya 2021.

Bingwa huyo alishinda mashindano hayo pamoja na dereva mwenza Julien Ingrassia, baada ya kuwabwaga wenzao wa Toyota, Toyoya Gazoo na mwenzake Takamoto Katsuta, na dereva wa Hyundai Motorsport Ott Tanak ambaye alimaliza katika nafasi ya tatu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 073248269.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke