Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Raila Odinga aijia juu serikali ya Kenya kuhusu bei kubwa za mafuta

Cf07411ff1c14094 Raila Odinga aijia juu serikali ya Kenya kuhusu bei kubwa za mafuta

Fri, 17 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kinara wa chama cha Orange Democratic Movement (ODM) Raila Odinga Alhamisi, Septemba 16, alivunja ukimya wake kufuatia uamuzi wa serikali kuongeza bei ya mafuta.

Mamlaka ya Kudhibiti Kawi nchini (EPRA) mnamo Jumanne, Septemba 14, 2021, ilisema kwamba bei ya petroli, dizeli na mafuta ya taa imeongezeka kwa Ksh 7 kwa lita.

Katika taarifa yake kwenye Twitter, Odinga alibainisha kuwa ongezeko la gharama ya mafuta ni pigo kwa Wakenya ambao tayari wamefinywa na COVID-19Alilaani serikali kwa hatua hiyo akitoa wito kwa hatua za haraka kuchukuliwa ili kuwaokoa Wakenya na mzigo mzito wa kudora kwa uchumi

Katika taarifa yake kwenye Twitter, Odinga alibainisha kuwa ongezeko la gharama ya mafuta ni pigo kwa Wakenya ambao wanazama katika deni kutokana na athari za COVID-19.

Alilaani serikali kwa hatua hiyo akitoa wito kwa hatua za haraka kuchukuliwa ili kuwaokoa Wakenya na mzigo mzito wa kudora kwa uchumi.

Kiongozi huyo wa ODM alisema kuwa Wakenya wanajitahidi kila kuchao kutafuta lishe na kuongezeka kwa bei ya mafuta kutapelekea kupanda kwa bei ya bidhaa ndogo ndogo.



Read also

Magazeti Ijumaa: Rais Uhuru na DP Ruto Walitumiana Jumbe za Makasiriko

"Wakenya wamekuwa wakihangaika kutafuta lishe tangu kuanza kwa janga hilo na sasa ongezeko a mafuta ya bei hujeda likawaumiza hata zaidi. Bei ya mafuta inapaswa kushukishwa haraka iwezekanavyo ili kumuokoa mwananchi wa kawaida," taarifa yake ilisema.

Mamlaka ya Kudhibiti Kawi nchini (EPRA) mnamo Jumanne, Septemba 14, 2021, ilisema kwamba bei ya petroli, dizeli na mafuta ya taa imeongezeka kwa Ksh 7 kwa lita.

Bei ya petroli jijini Nairobi ilipanda kutoka KSh 134.72 hadi KSh 127.14, bei ya dizeli ikawa KSh 115.60 kutoka KSh 107.66 nayo bei ya mafuta taa ikiongezeka kutoka KSh 97.85 hadi KSh 110.82.

Baada ya EPRA kutangaza bei mpya za mafuta, Muungano wa Wafanyakazi Nchini Kenya (COTU) ulijitokeza kulaani hatua hiyo ya serikali.

Kupitia kwa Katibu Mkuu Francis Atwoli muungano huo ulipinga kuongezeka kwa bei ya mafuta na kumtaka Rais Uhuru kujitoeza na kuzungumzia swala hilo ambalo limewakera wananchi.

Naibu Rais William Ruto pia aliwataa washikadau katika sekta hiyo kuandaa mkutano na wabunge ili kupata suluhu la kudumu kuhusu ongezeko hilo.

"Nataka kuwauliza wale wote ambao wamepewa majukumu na Rais Uhuru Kenyatta kuchukua hatua ya haraka na kutoa ushauri kwa serikali ili maamuzi sahihi yafanywe ndiposa hali idhibitiwe," Ruto alisema.

Ruto alizungumza katika makazi yake rasmi ya Karen Alhamisi, Septemba 16, wakati wa mkutano na wajumbe wa United Democratic Alliance (UDA) kutoka Kandara, kaunti ya Murang'a.

Awali, madereva na wahudumu wa bodaboda walifurika katika mji wa Migori kuandamana Alhamisi, Septemba 16 kulalamika kuongezeka kwa bei ya mafuta nchini.

Shughuli mjini humo zilikwama huku waandamanji hao wakifunga barabara wakitumia mawe na matairi ya magari huku polisi wakiwatazama kwa mbali.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke