Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Punguza bangi, Khalighraph amjibu Bahati

736fec4d23eec02d Punguza bangi, Khalighraph amjibu Bahati

Wed, 9 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Bahati aliachia kibao kwa jina Fikra Za Bahati, ambapo alikuwa anawarushia vijembe wasani kadhaa katika tasnia hiyo

- Muimbaji huyo alidai kuwa Khaligraph Jones anatumia dawa za kusisimua misuli kupata matokeo bora kwenye gym

- Rapa huyo alimjibu akimshauri awache kutumia mihadarati na atulie

Khaligraph Jones amemjibu Bahati ambaye alimrushia vijembe kupitia kibao cha Fikra Za Bahati alichoachia Jumanne, Juni 8.

Muimbaji huyo wa zamani wa nyimbo za injili amekuwa akipika kibao kipya studioni ambacho aliachia wimbo wa kwanza kutoka kwa albamu yake mpya.

Katika kibao hicho, Bahati aliwarushia vijembe wasanii tajika wakiwemo Sauti Sol, Ringtone, Octopizzo, Daddy Owen na wengine.

Pia alimtaja Khaligraph Jones akidai anatumia dawa za kusisimua misuli kupata matokeo bora kwenye gym.

Akimjibu Bahati, Khaligraph alipakia picha yake akiwa ametindinya misuli akiwa na rafiki yake nchini Marekani, ambapo amekuwa akipiga shoo kwa siku kadhaa.

Rapa huyo aliyevuma na wimbo Tuma Kitu alidai kuwa Bahati ameanza kutumia dawa za kulevya na kuimba matusi. Alimshauri awache kutumia mihadarati na atulie.

Bahati pia kwa utani alimjibu Khaligraph akisema "Kweendaaa Mi sikuogopi (sic)."

Majibu hayo yaliwavunja mbavu wafuasi ambao wanatumaini kuwa Khaligraph atatunga wimbo wa kumchongoa Bahati.

Bahati Avuta SigaraWimbo huu umeachiwa siku moja baada ya Bahati kupakia video yake akivuta sigara kubwa.

Video hiyo iliyopakiwa Juni 7, 2021, inamuonyesha Bahati akiwa amevalia suti na miwani ya jua akivuta sigara huku mwanamke akiwa amesimama kando yake.

Katika jumbe, Bahati alifichua kuwa video ni kutoka kwa kibao chake ambacho atawachia Juni 8.

Video hiyo iliibua hisia mseto miongoni mwa wafuasi wake huku wengi wakikumbuka maisha yake ya awali akiwa mwanamuziki wa injili.

Katika mahojiano ya awali na MC Jessy, muimbaji huyo alisema huenda atagura kuimba nyimbo za injili akidai sekta hiyo imeoza.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke