Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Proffesor Hamo asema atamuoa Jemutai kama mke wa pili, adai wametoka mbali

Ff58fd526f9a76ff Proffesor Hamo asema atamuoa Jemutai kama mke wa pili, adai wametoka mbali

Wed, 26 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Wachekeshaji Professor Hamo na Jemutai huenda wakafufua penzi lao baada ya kutatua tofauti zao

- Hamo amesema yuko tayari kumuoa Jemutai kama bibi wake wa pili kwa sababu anampenda

- Kulingana na Hamo, watu wanaogombana ndio wanaopendana na anaamini mapenzi ya dhati yapo

- Jemutai alimuanika Hamo mitandaoni kwa kuwatelekeza watoto wao wawili

Mchekeshaji wa Churchill Show Proffessor Hamo na Jemutai huenda wakafufua tena penzi lao baada ya kutatua tofauti zao hivi majuzi.

a

Wawili hao kwa zaidi ya mwezi mmoja uliopita, wamekuwa gumzo kwenye mitandao ya kijamii baada ya kuanika uchi wa penzi lao.

Ilianza na Jemutai kumkashifu Hamo kwa kuwatelekeza watoto wao wawili, kutolipa kodi ya nyumba kwa zaidi ya miezi mitano na mambo mengineyo.

Kwa upande wake, Hamo aliagiza watoto hao wafanyiwe DNA kabla ya kuwawajibikia kama baba yao mzazi.

Baada ya matokeo, ilibainika kwamba alikuwa baba halali wa watoto hao. Hata hivyo, Hamo alijutia hatua hiyo na ikamulazimu amuombe Jemutai msamaha na mashabiki wake kwa jumla.

Kwa sasa, Hamo amesema yuko tayari kumuoa Jemutai kama mke wa pili akidai kwamba wametoka mbali, hii ni baada ya shabiki mmoja kumuuliza ana mpango gani baada ya sarakasi hiyo kutokea.

" Umetatua tofauti zako na Baby Mama", Shabiki mmoja alimuuliza.

Akimjibu, Hamo alisema, " Jemutai sio Baby Mama ila ni mke wangu."

Shabiki mwingine aliuliza," Utafufua penzi lako kwa Jemutai,?

" Watu wanaopendana ndio hugombana," Hamo alimjibu Shabiki huyo.

Kama ilivyoripotiwa awali, Hamo aliahidi kuwalea watoto wake wote na kwamba siku moja watamsamehea watakapogundua sarakasi iliyotokea kati yake na mama yao.

" Kwa watoto wangu, maisha sio rahisi, Baba yenu anajutia na anaomba radhi, anatumai siku moja mkiwa wakubwa mtaelewa jinsi maisha yalivyo, najua mtanisamehea.Nawapenda wote na nitasimama na nyinyi katika hali zaote," Hamo alisema.

TUKO.co.ke inafahamu kwamba Proffessor Hamo ana mke mwingine ambaye anaishi mjini Nakuru na kwa pamoja wamejaliwa watoto watatu.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke