Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Prof Hamo apigwa kalamu Hot 96 FM

E27a1b597f26b17b Prof Hamo apigwa kalamu Hot 96 FM

Thu, 13 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Profesa Hamo alipigwa kalamu kutoka redio ya HOT 96 ambapo alikuwa mtangazaji wa kipindi cha asubuhi

- Duru zinaarifu kuwa mcheshi huyo hajaripoti kazini kwa wiki tatu na hakuwasiliana na wakubwa wake

- Ilidaiwa hakupokea simu kutoka afisini ikiwemo ile ya mtangazaji mwenza

Shirika la Royal Media Services (RMS) limemfukuza kazi mcheshi wa kipindi cha Churchill Live na mtangazaji wa kipindi cha HOT 96 FM asubuhi Profesa Hamo.

Haya yanajiri siku moja baada ya matokeo yaliyotarajiwa ya DNA kuthibitisha kuwa alizaa watoto wawili na mchekeshaji mwenzake, Jemutai.

Mchekeshaji huyo wa Churchill Show alidaiwa alikataa kuwajukumikia wanawe hadi uchunguzi wa DNA ufanyike.

Hamo pia amemuoa mwanamke mwingine huko Nakuru, na wana watoto watatu pamoja.

Amezua gumzo mitandaoni kwa wiki mbili zilizopita baada ya mama wa watoto wake kujitokeza na kuomba msaada akidai kwamba Hamo aliwatoroka.

Duru za kuaminika kutoka shirika hilo zilisema Hamo amesusia kazi kwa wiki tatu pasi na kumjulisha yeyote aliko na sababu za kuchukua hatua hiyo.

Aidha ilisemekana juhudu za kumtafuta kutoka kwa wakubwa wake hazikufua dafu kwani hakuwa akipokea simu hata zile za mtangazaji mwenze Jeff Koinange.

Hamo hajakuwa akisikika hewani kwa muda sasa suala ambalo liliwaacha wengi na masuali chungu nzima iwapo alijiuzulu.

Wapenzi hao waliotengana walianza kuchafuliana majina hadharani baada ya Jemutai kufichua kwamba Hamo aliwatembelea watoto wake mara ya mwisho mnamo Oktoba 2020 kabla ya kuhama Nairobi.

Tangu wakati huo, amekuwa akiwalea watoto wao pekee yake.

Hata hivyo Hamo, kwa upande mwingine, alipuuzilia mbali madai hayo na kudumisha kuwa yeye hajawakataa watoto wake.

Hamo bado hajazungumza lolote kuhusu hatua ya kufutwa kazi.

Awali Jemtua alifichua kwamba kw awakati mmoja alichukua mkopo wa KSh 30,000 kuwalipia watoto wa Hamo karo ya shule.

"Wakati wote ule nilikuwa ninawanunulia watoto wangu bidhaa nilikuwa nawakumbuka wale watoto wake wengine. Niliwalipia karo watoto wake na vile vile ada ya kukodisha nyumba ya mkewe wa kwanza Nakuru, "Jemutai alisema.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke