Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Penzi la rapa Juliani na Lilian Nganga lazidi kushine

7d0d455880c5d064 Penzi la Juliani na Lilian Nganga lazidi kuchanua, wawili hao wazuru Kisumu

Wed, 17 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Penzi kati ya rapa Juliani na aliyekuwa mke wa Gavana wa Machakos Alfred Mutua Lilian Nganga linazidi kuchanua. Juliani na Lilian Nganga wamezua gumzo mitandaoni baada ya kupakia picha zao wakiwa maeneo ya Magharibi mwa Kenya.

Wachambuzi wa mitandao wanaamini wawili wao walipiga picha hizo wakiwa mkoa wa Kisumu walikozaliwa wazazi wa Juliani.

Baadhi ya mashabiki wao walidadisi kwamba huenda Juliani alikuwa amempeleka Lilian kumtambulisha kama mke.

" Nimekuwa nikitembea mguu tupu, hii inaitwa 'Earthing', kuondoa machungu kwenye ardhi na kupokea nguvu za uponyaji kutoka kwenye ardhi. Ili kupanda mbegu lazima ife ili imee upya," Juliani aliandika.

Lilian pia aliposti picha kadhaa akiwa sehemu aliyokuwa pamoja na Juliani akidai kwamba anapunga hewa safi na kufurahia mazingira mazuri.

Esther Musila Afichua Mengi Kuhusu Penzi Lake kwa Msanii Guardian Angel

Haya hapa baadhi ya maoni ya Wakenya;

@leonard_lucerna:

“ Najua hapa ni Kisumu, karibu nyumbani Mama".

@okothlyn:

“Luoland inapendeza sana, karibu nyumbani shemeji.”

@Lillykish:

“ Umempeleka Lilian nyumbani kumsalimu mama mkwe?".

@faithsaginna:

“ Mimi hukufurahia sana, mara mingi huwa unanitia moyo ninapotaka kukata tamaa."

@janoy69:

“Karibu nyumbani, wasipende wapende, mapenzi hushinda,"

Hivi maajuzi, Lilian ambaye alikuwa katika ndoa kwa miaka 10 na gavana Mutua, alimkashifu kwa kumpokonya gari lake na kuliuza, pia alikuwa amemtaka amrejeshe pesa zote mbazo aliwahi kumpea.

Lilian alisema hana deni lolote na gavana huyo akiongezea kwamba aliondoka nyumbani kwake na nguo zake tu bila chochote.

" Nilipoondoka nyumbani kwake mwezi Juni mwaka huu, nilibeba nguo zangu pekee, sina chochote cha kumrudishia. Nina kampuni yangu ya usafiri na salon ambazo mimi mwenyewe nilitia bidii kuzipata," Lilian alisema.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke