Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muimbaji Bahati amkumbatia "shetani" na drama zingine zilizoshuhudiwa wiki hii

9d3601369b8f5bd8 Muimbaji Bahati amkumbatia "shetani" na drama zingine zilizoshuhudiwa wiki hii

Thu, 10 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kila siku ya wiki, TUKO.co.ke inakupakulia kwa mukhtasari matukio na habari muhimu zilizogonga vichwa vya habari wiki hii ili ukapate kufahamu kwa upana na utendeti mambo yalivyo ulimwenguni.

1. Video ya Muimbaji Bahati Akivuta Sigara Yawachanganya Wafuasi wake

Bahati aliibua mjadala moto kwenye mtandao wa kijamii baada ya kupakia video yake akivuta sigara.

Kutokana na namna alikuwa anapiga mapafu, ni dhahiri kwamba ana weledi wa kuvuta sigara.

2. Rais wa Ufaransa Emmanuel Macron Azabwa Kofi Moto na Raia Hadharani

Kisa hicho kilitokea wakati Macron alikuwa ametembelea eneo la Drome kusini mashariki mwa Ufaransa ambapo alikuana na wahudumu wa hoteli na wanafunzi.

Alikuwa ametoa mkono wake kumsalimu jamaa huyo ambaye aligeuka na kumzaba kofi kiongozi wa taifa.

3. Rais Asiyeheshimu Sheria! Maraga Asema Atakavyo Kumbuka Uhuru

Aliyekuwa jaji mkuu David Kenani Maraga alimshambulia Rais Uhuru Kenyatta kutoka na hatua yake ya kukosa kuwateua majaji sita waliopendekezwa na tume ya huduma za mahakama JSC.

Kwenye mahojiano na runinga ya KTN, Maraga alisema Rais Uhuru ataacha sifa za kiongozi wa taifa ambaye alikaidi katiba.

4. TB Joshua: Mhubiri Maarufu Kutoka Nigeria Afariki Dunia

Mtumishi wa Bwana maarufu kutoka nchini Nigeria TB Joshua alifariki dunia.

TB alifariki dunia Jumamosi Juni 5 ingawa taarifa kuhusu kiini cha kifo chake zingali hazijafahamika.

Joshua alikuwa ni mtumishi wa Bwana maarufu na mwenye ushawishi mkubwa kwa wafuasi wake ndani na nje ya mipaka ya Lagos.



5. Mama Kutoka Afrika Kusini Ajifungua Watoto 10, Avunja Rekodi ya Ulimwengu

Mwanamke Afrika Kusini alijifungua watoto 10 kwa mpigo na kuvunja rekodi ya ulimwengu ambayo ilikuwa imewekwa na mwanamke kutoka Mali aliyepata watoto tisa miezi kadhaa iliyopita.

Gosiame Thamara Sithole mwenye umri wa miaka thelathini na saba alijifungua watoto hao kumi usiku wa Jumatatu, Juni 7.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke