Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Muigizaji wa Papa Shirandula, Njoro ashangalia baada ya bintiye kupata B-

Af5bd1c6c677c84f Muigizaji wa Papa Shirandula, Njoro ashangalia baada ya bintiye kupata B-

Tue, 11 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Muigizaji Njoro ni miongoni mwa maelfu ya wazazi Wakenya ambao wanasherehekea matokeo ya KCSE yaliyotangazwa Jumatatu, Mei 10

- Binti yake Njoro alikuwa miongoni mwa watahiniwa 366,834 wa kike ambao walifanya mtihani huo

- Alipata alama ya B-

Muigizaji wa Papa Shirandula Ken Gichioya almaarufu Njoro, anajivunia kuwa baba baada ya mtoto wake wa pili Natalie Waithera kuwa miongoni mwa watahiniwa 741,161 waliofanya Mtihani wa Kidato cha Nne 2020.

Kati ya watahiniwa hao 747,161, 366,834 walikuwa wasichana na wengine 380,327 wavulana.

Natalie alipata alama ya B- huku baba yake akisherehekea matokeo hayo pamoja na wafuasi wake kwenye mtandao wa kijamii akimsifu kwa kuinua jina lake.

"Asante Mungu! Maombi yenyu hayakuwa ya bure! Tumepata B-.Hongera binti yangu mpendwa umenifanya kujivunia." alisema Njoro.

Waigizaji wenzake Njoro na wafuasi wake walijiunga naye katika kusherehekea matokeo ya binti yake na hii hapa maoni yao.

jackyvike aliandika: "Yaaaay! KongoleNatalie."

daisynetia: "Yay, hongera Natalie Mungu akubariki ma'am."

nyaminde: "Hongera Natalie!! Naona tutakuwa na daktari kwa familia."

kajairo: "Hongera kaka. Mungu amewatendea."

Takwimu za Knec zinaonyesha kuwa watahiniwa 752,933 walisajiliwa kufanya mtihani wa KCSE mwaka uliopita katika vituo 10,437.

Akizungumza akiwa katika jumba la Mitihani House Jumatatu , Mei 10, Magoha aliwatambulisha wanafunzi ambao wameboresha matokeo yao kutoka maksi 200 katika mtihani wa KCPE miaka minne baadaye.

Kwenye hotuba yake, Magoha alisema wanafunzi hao walivunja rekodi na kuwahakikishia wakenya kwamba sio lazima mwanafunzi ajiunge na shule ya kitaifa ndiposa aweze kujiunga na chuo kikuu.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke