Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mtangazaji Maina Kageni asema anapenda sana wanawake lakini hawezi kuoa

Ddda940dfa15761b Mtangazaji Maina Kageni asema anapenda sana wanawake lakini hawezi kuoa

Wed, 26 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Maina Kageni ni anatambuliwa sana kupitia shoo yake ya asubuhi ambayo huibua mdhahalo miongoni mwa wasikilizaji wake

- Maina anapenda sana kuwaunga mkono wanawake huku mtangazaji mwenzake akiwatetea wanaume wakizungumzia masuala ya mahusiano

- Maina, ambaye amekuwa kwenye ulingo wa utangazaji kwa miaka 20, ana mashabiki wengi na wafuasi kwenye mtandao wa kijamii

Mtangazaji wa Classic 105 FM Maina Kageni ni mtu tajika Kenya. Kageni ambaye ana talanta katika nyanja ya utangazaji amehudumu kwa miaka 20 na ana mashabiki wengi na wafuasi kwenye mtandao wa kijamii

Maina huandaa shoo ya asubuhi pamoja na Mwalimu King'ang'i, ambapo huwa wanazungumzia masuala ya ndoa na mahusiano. Anapenda sana kuwaunga mkono wanawake huku mtangazaji mwenzake akiwatetea wanaume

Akizungumza katika mahojiano na mcheshi Jalang'o, Maina alisema anapenda sana wanawake.

"Wanawake hujenga maboma sio manyumba," alisema Maina.

Akizungumzia ndoa, Maina alisema hataoa kwa sababu ametambua kupitia shoo yake ya asubuhi kuwa ndoa si ya kila mtu.

"Baadhi ya vitu mimi husikia kwenye shoo kuhusu ndoa ni vya kutisha. Imenifunza kitu moja ndoa si ya kila mtu lakini usiwahi huwezi..," Maina alisema.

Aliongezea kuwa: "Kile wanaume wanafanya ni kujaribu kuwafurahisha wanawake. Unawafanyia vitu ambavyo unafikiria watakumbuka milele. Hivyo ndio vile mnajiua"

Mtangazaji huyo wa radio alisema anapenda kuwa huru na anaweza kufanya kila kitu anataka na kusafari kila mahali bila kuomba ruhusa.

"Mimi nina shida ya kuomba ruhusa kufanya kitu nataka," Maina alisema.

Maina anapenda kuficha familia yake akisema ni kwa sababu hawapendi kuwa maarufu.

Kama ilivyoripotiwa awali, Maina amekuwa akichapisha picha za mvulana ambaye anamfanana na kuwacha wafuasi wake na maswali endapo ni mtoto wake.

Kulingana na duru, mtoto huyo ni wa Maina wa kupanga wengine wakidai ni mpwa wake lakini hajawahi kufichua habari zaidi kuhusu madai hayo.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke