Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mpenzi wa Mchekeshaji Kansiime amposa miezi michache baada ya kujifungua

52f09728bb1810a0 Mpenzi wa Mchekeshaji Kansiime amposa miezi michache baada ya kujifungua

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mchekeshaji Anne Kansiime na mpenzi wake Skylanta huenda wanapanga kufunga ndoa hivi karibuniHii ni baada ya Syklanta kumposa Kansiime miezi mitatu baada ya wapenzi hao wajaliwa mtoto wao wa kwanzaWapenzi hao wamekuwa wakichumbiana tangu mwaka wa 2018 na wamekuwa wakionyesha penzi lao hadharani mitandaoniMchekeshaji maarufu kutoka Uganda Anne Kansiime ameposwa na mpenzi wake takriban miezi mitatu baada ya kujaliwa mtoto wao wa kwanza.

Kansiime akiwe mwenye furaha, alionyesha pete yake ya kuposwa kupitia mtandao wa Instagram na kumuahidi Syklanta kwamba atampenda kwa kila hali na kwamba pia penzi lao litadumu milele.

" Nimepata penzi la kweli kwako wewe Skylanta, naahidi kukupenda milele, asante kwa kukuwepo kila ninapokuhitaji," Alisema Kansiime.

" Asante kwa kunielewe jinsi nilivyo hasa na huu wazimu wangu. Nitakupenda milele," Aliongezea Kansiime.

Kansiime na mpenzi wake walianza kuchumbiana mwaka wa 2018 baada ya kuachana na mume wake wa kwanza Gerald Ojuol mwaka wa 2017.

Ojuok na Kansiime walikaa katika ndoa kwa miaka minne ila hawakujaliwa mtoto.

Skylanta na Kansiime walijaliwa mtoto wao wa kwanza Aprili 24, 2021 na bila shaka wanafurahia penzi lao.

Awali, TUKO.co.ke iliripoti kwamba Kansiime alifiwa na mamake wiki chache zilizopita, hafla ya mazishi ilifanyika Juni 11, 2021.

Kansiime alisema kifo cha mamake kilikuwa cha kusherehekewa wala sio cha kuombeleza na kuhuzunisha.

" Tulimpa mama wetu heshima zake za mwisho kwa njia ya kipekee, hii ilikuwa ishara ya kutosha kusherehehea maisha yake hapa duniani, alikuwa zawadi na baraka kwa familia," Alisema Kansiime.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari zaidi kutoka TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke