Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

TV

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Marburg yapungua Rwanda

Ugonjwa Pic Marbug Marburg yapungua Rwanda

Fri, 18 Oct 2024 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

MAAMBUKIZI ya virusi vya ugonjwa wa Marburg nchini Rwanda yamepungua baada ya watu waliokuwa hatarini kuanza kupatiwa chanjo.

Waziri wa afya nchini Rwanda Sabin Nsanzimana amesema tangu serikali kwa kushirikiana na kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika CDC kutoa chanjo maambukizi ya ugonjwa huo yamepungua katika ukanda huu wa Afrika Mashariki.

Hatahivyo,Mkuu wa Kituo cha kudhibiti na kuzuia magonjwa Afrika CDC Jean Kaseya amesema licha ya kupungua kwa maambukizi ya virusi vya ugonjwa wa Marburg kwa sasa wanakabiliana na tatizo la Mpox ambalo limeshafika katika nchi sita Barani Afrika.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live