Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Ladies Man: Picha za Omar Lali akifurahia muda na watalii wa kike

6553952fa9d538ef Ladies Man: Picha za Omar Lali akifurahia muda na watalii wa kike

Sun, 1 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Lali kwa sasa ni celeb tangu agonge vichwa vya habari kutokana na kifo cha Tecra Muigai ambaye ni bintiye bwanyenye Tabitha KaranjaKwa sasa anakabiliwa na kesi kuhusu kifo cha Tecra huku familia ya Tabitha ikishuku alihusika katika majeraha ya bintiyeLali huwavutia mabinti kutokana na kimo chake, ustadi katika matumizi ya boti na pia huwa ni mtu mwenye gumzo za kuvutiaWanamtandao wamefurahishwa na picha za Beach Boy Omar Lali ambaye anaonekana kuwavutia watalii wa kike sana kwenye shughuli zake.

Lali amekuwa ni msanii sasa tangu agonge vichwa vya habari kutokana na kifo cha mwanawe bwanyenye Tabitha Karanja wa Keroche Breweries Tecra Muigai.

Lali walikuwa wakijivinajri na Tecra kwenye mojawapo wa visiwa katika ukanda wa Pwani wakati binti huyo alipata majeraha na kukimbizwa hospitali.

Hata hivyo hakupona majeraha aliyokuwa amepata na Lali akakamatwa akihusishwa na kifo hicho na kesi ingali inaendelea.



Hat hivyo, licha ya kusema kifo cha mpenziwe lilikuwa pigo kubwa maishani Lali ameamua kupiga moyo konde na kuendelea na masiha.



Read also

Ifahamu Sababu ya Makurutu Kukaguliwa Meno Kabla ya Kujiunga na Vikosi vya Polisi

Meza ya TUKO.co.ke ilipata duru kuwa Lali anaendelea na maisha yake katika visiwa vya Lamu kama alivyokuwa kabla ya kukutana na Tecra.

Kulingana na wanaomjua, umaarufu wake umepandwa kutokana na kesi hiyo huku wengi wa watalii wa kike wakimsaka kama simba wanavosaka windo jangwani.



Jumamosi Julai 30 wanamtandao walimiminika mtandaoni kumsifia Lali baada ya kuonekana na kipusa mwingine.

Kulingana na picha zilizochapishwa katika mtandao, dume huyo alikuwa akimkaribisha mtalii huyo baada ya kutua katika uwanja wa ndege.

Mafisi walisema weledi wa Lali katika kuwateka mabinti wenye sura, umbo na mifuko mizito ni jambo la kutamaniwa na wanaume ambao huwa kibarua kupata wa kuwapenda.

Jamaa mmoja wa familia alisema Lali huwavutia mabinti kutokana na kimo chake, ustadi katika matumizi ya boti na pia huwa ni mtu mwenye gumzo za kuvutia.

Amejifunza lugha nyingi zikiwamo Kijeremani na Kitaliano na hivyo kuwa rahisi kuwateka watalii wasioelewa Kiswahili na Kiingereza.

READ ENGLISH VERSION



Read also

Picha Tamu za Christine Ambani Aliyeuawa Ndani ya Lojing'i Githurai

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke