Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenyatta ahofia usalama, Rais amuagiza Waziri

Kenyatta 1140x640.jpeg Kenyatta ahofia usalama, Rais amuagiza Waziri

Mon, 31 Oct 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Umoja wa Afrika AU, umetoa wito wa kusitishwa mara moja mapigano yanayoongezeka nchini Jamhuri ya Kidemokrasia ya Kongo, huku Rais wa Angola Joao Lourenco akisema atamtuma Waziri wake wa Mambo ya Nje, Tete Antonio nchini DRC ili kupatanisha mzozo huo.

Rais mstaafu wa Kenya, Uhuru Kenyatta ambaye ni Mjumbe wa Umoja huo na Mpatanishi wa Jumuiya ya nchi za Afrika Mashariki kuhusu mzozo huo, amesema ana wasiwasi juu ya hali ya mashariki mwa Kongo, na kuzitaka pande zote kuheshimu sheria za kimataifa, usalama wa raia na utulivu katika mipaka ya nchi za ukanda huo.

Hata hivyo, hatua hiyo inajiri ikiwa siku chache baada ya DRC kumtimua Balozi wa Rwanda nchini humo, Vincent Karega kufuatia tuhuma za muda mrefu kuwa Kigali inawaunga mkono waasi wa M23.

Rwanda, ambayo inakanusha shutuma hizo imeelezea kusikitishwa kwake na uamuzi huo na kuongeza kuwa wanajeshi wake kwenye mpaka wa nchi hizo mbili wako kwenye tahadhari kubwa.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live