Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Kenya yajizolea medali nyingi kwenye Riadha za U-20

0e5095d859ae24c3 Kenya yajizolea medali nyingi kama njugu kwenye Riadha za U-20

Mon, 23 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Kenya imefanikiwa kuonesha ugwiji wake kwenye Riadha za Dunia za vijana wasiozidi umri wa miaka 20 huku ikiongoza kwenye chati ya kuzoa medali nyingi.

Ukingo wa mashindano hayo ulishuhudia timu ya Kenya ikishinda medali tatu ya dhahabu, Emmanuel Wanyonyi aking'aa kwenye mbio za mita 800 Purity Chepkirui na Amos Serem ndio baadhi ya wanariadha walioibuka shujaa kwenye fainali za mashindano hayo Jumapili, Agosti 22, katika Uchanjio wa Michezo wa Moi, Kasarani Kenya inaongoza kwenye chati ya medali katika mashindano yaliyokamilika ya Riadha za Dunia za vijana wasiozidi umri wa miaka 20.

Kenya, ambayo ilikuwa mwenyeji wa makala hayo ya 2021, ilizoa medali 16.

Kati ya medali hizo 16, nane ni za dhahabu, moja ya fedha na saba za shaba.

Ukingo wa mashindano hayo Jumapili, Agosti ulishuhudia timu ya Kenya ikishinda medali tatu ya dhahabu, Emmanuel Wanyonyi aking'aa kwenye mbio za mita 800, Purity Chepkirui, na Amos Serem wakimaliza wa kwanza katika mbio mbalimbali.



Finland ilimaliza ya pili kwenye chati ya medali baada ya kushinda jumla ya medali tano, nne zikiwa za dhahabu, huku Nigeria ikikamilisha mdwara wa tatu bora.

Mataifa mengine ambayo yaliyong'aa ni pamoja na Ethiopia, Jamaica, na Afrika Kusini ambayo yalipata medali tatu za dhahabu kila mmoja.

Benson Kiplangat ashindia Kenya medali ya kwanza ya dhahabuAwali, TUKO.co.ke iliripoyia namna mnamo Alhamisi, Agsti 19, Benson Kiplangat alishndia Kenya medali yake ya kwanza ya dhahanu katika Riadha za Dunia za vijana wasiozidi umri wa miaka 20.

Mkenya huyo aliweka Kenya katika ramani ya dunia baada ya kushinda mbio za mita 5000.

Kiplangat alimaliza mbio hizo kwa weledi na kumlazimu Muethiopia Tadese Worku, aliyeshinda medali katika mbio za 3000 usiku uliotangulia kuridhika na medali ya fedha.

Levy Kibet, ni Mkenya mwingine ambaye alishiriki katika mbio hizo na kumaliza katika nafasi ya tatu na kushinda medali ya shaba.

Kenya yamaliza kidedea kwenye Tokyo Olympics Matokeo hayo ya kuridhisha ya Kenya yanakujia siku chache baada ya kuongoza bara Afrika wakat wa mashindano ya Tokyo Olympics.

Wakati huo Wakenya walifaulu kubeba medali 10 na kumaliza wa kwanza kwenye chati ya medali Bara Afrika.

TUKO.co.ke iliripoti kuwa medali hizo 10 ziliorodhesha Kenya kwenye nafasi ya 19 duniani huku Marekani ikiongoza.

China, Japan, na Uingereza pia yalitawala nafasi za tano bora.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke