Wafanyakazi wote wa kampuni ya umeme nchini Kenya kukaguliwa.
Hatua hii inakuja baada ya madai ya rushwa dhidi ya baadhi ya wafanyakazi.
Hivyo wafanyakazi wa kampuni ya umeme 'Kenya Power' wanapaswa kukabidhi kadi zao za benki na taarifa za akaunti zao za fedha za simu ifikapo Jumatatu.
Mali zote zinazomilikiwa na wafanyakazi pamoja na wenzi wao pia zitachunguzwa.
Kampuni imeanzisha msako huo baada ya taarifa kuvuja mtandaoni kuwa wafanyakazi huwa wanauza umeme kwa wateja kwa njia isiyo halali.
Kenya Power iko katika mchakato wa kuiboresha huduma za umeme na kupunguza gharama za huduma hiyo.