Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Jeff Koinange ashtushwa na ujuzi wa mwanawe kwenye soka

Eaaef0b46c5f70eb Jeff Koinange ashtushwa na ujuzi wa mwanawe kwenye soka

Thu, 15 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Katika video aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram Jeff alijivunia namna mwanawe ni mweledi wa kupepeta mpira

- Mtangazaji huyo tajika aliwaomba wafuasi wake kusambaza video hiyo kuonyesha ujuzi wa mwanawe

- Jeff pia alishirikisha vilabu vikuu duniani kwenye video hiyo ikiwemo Liverpool, Manchester United na Chelsea kushuhudia weledi wa mwanawe kwenye soka

Ni matumaini ya kila mzazi kumuona mwanawe akifaulu maishani kupitia talanta na pia masomo.

Haya si tofauti na maazimio ya mwanahabari wa Citizen TV, Jeff Koinange kwa mwanawe Jamal Mbiyu Koinange ambaye alisifia ujuzi wake kwenye ulingo wa soka.

Katika video aliyochapisha kwenye ukurasa wake wa Instagram siku ya Jumatano, Aprili 14, Jeff alijivunia namna mwanawe ni mweledi wa kupepeta mpira.

Mtangazaji huyo tajika aliwaomba wafuasi wake kusambaza video hiyo huku akishirikisha vilabu vikuu duniani ikiwemo Liverpool, Manchester United na Chelsea kushuhudia talanta ya mwanawe.

"Hii ni talanta tupu! Hongera, kijana! Najivunia kwako sana. Tangaza ujumbe! aliandika Koinange.

Mwanahabari mwenzake Victoria Rubadiri pia alishindwa kuzuia furaha yake huku akifurahia talanta ya kipekee ya Jamal.

Viatu Vinavyofanana Miguu ya Binadamu Vyaibua Zogo Mtandaoni

Kwingineko kwenye nyanja ya uanahabari, Mhariri wa video katika Shirika la Utangazaji la Kenya (KBC) Betty Barasa ambaye aliuawa na majambazi alizikwa nyumbani kwake eneo la Oloolua, Ngong, Jumatano, Aprili 14.

Programu ya hafla ya mazishi yake ilionesha kuwa ibada ilifanyika katika makafani ya Montezuma kabla ya mwili kupelekwa Oloolua kwa safari yake ya mwisho.

Mwanahabari huyo aliuawa kwa kupigwa risasi nyumbani kwake mnamo Aprili 7, na Majangili waliokuwa wamejihami kwa bunduki na ambao walimpiga risasi na kumuua walikuwa wamefunika nyuso zao walipokuwa wakitekeleza uhayawani huo.

Polisi wanasema hamna mtu yeyote aliyekamatwa hadi sasa kuhusiana na kisa hicho lakini uchnguzi bado unaendelea.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke