Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Huu ndio uhusiano mrefu kuwahi kuwa nao, Sidika akiri kuwezwa na penzi la Mauzo

B3c233c70320ff10 Huu ndio uhusiano mrefu kuwahi kuwa nao, Sidika akiri kuwezwa na penzi la Mauzo

Mon, 7 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Vera Sidika na mpenzi wake Brown Mauzo wamekuwa wakiishi pamoja mjini Mombasa tangu janga la COVID-19 kulipuka duniani 2020

- Wamekuwa wakiishi kama wanandoa na mashabiki wao wana imani kuwa ndoa yao itadumu kwa muda mrefu

- Vera aliingia katika mahusiano ya kimapenzi na Mauzo miezi michache baada ya kuvunjika kwa uhusiano wake na daktari Mtanzania Jimmy Chansa

- Sosholaiti huyo alifichua kuwa angelipenda kuwa na watoto watatu

Sosholaiti Vera Sidika na mahabubu wake Brown Mauzo wataadhimisha mwaka mmoja wa mahusiano yao hivi karibuni. Wapenzi hao wamekuwa wakiishi pamoja mjini Mombasa tangu janga la COVID-19 kulipuka duniani 2020.

Vera amewezwa na penzi la Mauzo huku akifichua kwa mara ya kwanza kuwa uhusiano wake na muimbaji huyo kutoka Pwani ndio umedumu kwa muda mrefu ikilinganishwa na mahusiano yake ya awali.

Akimjibu shabiki ambaye alitaka kujua ni lini atasherehekea maadhimisho ya ndoa yake na Mauzo alisema:

"Agosti 12, 2021, ni maadhimisho yetu ya kwanza. Huu ndio uhusiano mrefu ambao nimewahi kuwa nao na usiokuwa na matatizo. Hakuna visanga."

Aliongezea kuwa "Mahusiano yangu ya zamani yamekuwa ya miezi sita lakini wakati huu nitajua endapo kuna hatma au la. Sipendi kupoteza muda wangu nikiona hakuna hatma huwa ninakatiza tu"

Akiulizwa endapo huchungulia simu ya mpenzi wake Vera alisema:

"Huwa unachunguza tu simu ya mwanamume wako wakati tu hamuamini ama endapo unamshuku anakudangaya."

Sosholaiti huyo pia alifichua kuwa angelipenda kuwa na watoto watatu.



Katika taarifa ya awali ya TUKO.co.ke, Vera aliwashauri wanawake kukoma kuchumbiana na waume za watu akisema ni kizingiti katika kufaulu maishani.

Katika mazungumzo ya moja kwa moja na wafuasi wake kwenye Instagram, mmoja wa wafuasi wake alitaka kupata ushauri wa namna kukoma kuwa katika mahusiano na mume wa mtu.

"Mimi ni mpango wa kando wa mtu. Ninampenda sana nimeshindwa kumuacha."

Akimshauri mfuasi wake Sidika alisema:

"Na utabiki kuwa mpango wa kando daima.Mwanamume akisha lala nawe hawezi kufuata sana.Hata akikuwacha bado ataanza kuchumbiana na mwingine wewe ukibaki mpango wa kando. Hii ni kwa sababu amesha kupata na haogopi kukuwacha," alisema.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke