Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Harambee Stars yapanda hadi 102 kwenye orodha ya FIFA

E3911012abc269b8 Harambee Stars yapanda hadi 102 kwenye orodha ya FIFA

Thu, 8 Apr 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Kenya ilipanda hadi nafasi ya 102 kwenye orodha iliyotolewa na FIFA

- Waliopanda zaidi ni Guinea-Bissau baada ya kufuzu kuingia kampeni ya AFCON

- Harambee Stars wataanza kampeni yao ya kufuzu kwa Kombe la Dunia dhidi ya Uganda mnamo Juni 2021

Harambee Stars imepanda hatua mbili kwenye orodha ya hivi punde ya FIFA licha ya kubanduliwa kwenye mtanange wa Kombe la Afrika(AFCON).

Kenya ilipanda hatua mbili kutoka nafasi ya awali 104 hadi 102 katika viwango vya kimataifa na kushikilia nafasi ya 15 katika Bara Afrika.

Licha ya kushindwa kufuzu kwa AFCON, Kenya ilipiku baadhi ya mataifa kama vile Trinidad and Tobago na Palestine.

Kenya ilimaliza ya tatu Kundini G kwenye kampeni yao ya kufuzu kwa AFCON baada ya kupiga Togo 2-1 katika mechi ya mwisho ya makundi.

Waliingia katika mechi hiyo ya Togo wakijivunia droo ya 1-1 dhidi ya Misri kwenye mechi iliyosakatwa uwanjani Kasarani.

Katika orodha ya sasa, Harambee Stars pia ilishinda mechi mbili dhidi ya Tanzania na Sudan Kusini lakini mechi hizo hazikutambuliwa rasmi na FIFA.

Orodha ya sasa yaweka Kenya karibu na majirani wao Uganda, ambao wamepangiwa kuvaana kwenye kampeni ya kufuzu kwa Kombe la Dunia Juni.

Uganda wameorodheshwa kwenye nafasi ya 84 huku mahasidi wengine wa Kenya, Rwanda wakishikilia nafasi ya 129.

Senegal, ambao walifuzu mapema kwa AFCON mwaka 2020 wanashikilia nafasi yao Bara Afrika na wanafuatwa na Tunisia, Nigeria, Algeria na Morocco.

Msumbiji ndio wamepoteza zaidi kwa kushuka hadi nafasi ya 117 huku Guinea-Bissau wakipanda ngazi hadi 108.

Timu ambazo bado zinashikilia mduara wa sita bora ni Ubelgiji ambayo inaongoza Ufaransa, Brazil, Uingereza, Ureno na Uhisoania.

Italia walipanda hadi nafasi ya saba wakipiku Argentina na Uruguay.

Orodha nyingine itachapishwa Mei 27.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke