Naibu Rais Rigathi Gachagua amekanusha mashtaka yote 11 yanayomkabili akiwa mbele ya Bunge la Seneti ambaye pia aliandamana na mawakili wake.
Mashtaka hayo yalisomwa na karani wa Seneti Jeremiah Nyegenye leo siku ya Jumatano.
Sasa, kesi hiyo imefikia hatua ya kusikilizwa kikamilifu na kikao cha Bunge la Seneti.
Haya yanajiri baada ya Naibu Rais Rigathi Gachagua kushtakiwa na Bunge la Kitaifa kwa msururu wa tuhuma zikiwemo ufisadi, kumhujumu rais na kuendeleza mgawanyiko wa kikabila.
Bunge la Kitaifa lilipiga kura ya kumuondoa Gachagua madarakani ambapo wabunge 281 waliunga mkono hoja hiyo, huku 44 wakipiga kura kupinga na mmoja akikataa kupiga kura na hivyobasi kuafikia thuluthi mbili ya kura zilizohitajika ili kupitisha uamuzi wa kumuondoa afisini.
Bunge la Seneti limepanga siku mbili mfululizo za kusikiliza na kubaini hatima ya Gachagua.
Rigathi Gachagua anahitaji angalau maseneta 23 ili kunusurika kuondolewa kwake.