Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Eric Omondi amlilia mshindi wa "Wife Material 3" Monica Ayen amrudie

5298aa4202118ca6 Eric Omondi amlilia mshindi wa "Wife Material 3" Monica Ayen amrudie

Thu, 11 Nov 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Mchekeshaji Eric Omondi anajutia kuachwa na mwanadada wa shindano la Wife material 3 kutoka Sudan Kusini Monica Ayen na sasa anamlilia amrudie.

Omondi alimuandikia Ayen ujumbe mtamu na mzito kwenye mtandao wa Instagram alipokuwa akisherekea siku yake ya kuzaliwa, Novemba 11.

" Heri njema siku yako ya kuzaliwa mpenzi wangu, tafadhali rudi nyumbani, uje tutatue tofauti zetu, twende tukawaone wazazi na pia tuanzishe familia yetu," Omondi aliandika.

Akimjibu Omondi kwenye chapisho lake, kakake alimshauri Ayen aachane naye kwa sababu angali kwenye giza na hayuko tayari kwa ndoa.

Ayen alipoulizwa kwenye mahojiano iwapo anamchumbia Felix, alikana madai hayo na kusema kwamba wawili hao ni marafiki tu wa karibu na wa dhati.

Felix Omondi pia aliendelea na kumtakia Ayen heri njema siku yake ya kuzaliwa, Alisema" Furahia siku yako ya kuzaliwa mrembo, nakutakia maisha marefu pamoja nami. Achana na Eric ambaye ulimpa fursa ya kukuoa na hakuwa tayari. Sasa anakutaka umrudie. Kumbuka ni nani alikufanya usirudi Sudan Kusini wakati Eric alikumbwa na sarakasi nyingi. Hebu na asikukosee imani yako," Happy Birthday Jaber."

Awali, Ayen alikuwa amezungumzia sababu iliyomfanya amteme Eric akidai kwamba ni mkora na alimdanganya kuhusu mambo kadhaa pasipo yeye kujua alikuwa amefanya upelelezi kimya kimya.

"Eric ni muongo sana. Amenidanganya kuhusu mambo mengi. Mara ngapi nimemuuliza ataenda kuona wazazi wangu lini? Alikuwa ameniahidi tungeenda kuona wazazi Jumapili kwa kuwa ni siku ya sabato ila ilipofika akaniambia amesahau.

Swali tu ni kwamba utawezaje kusahau uko na mke kwa nyumba na mnafaa kuenda kuona wazazi wake. Mimi siwezi kuvumilia" Ayen alisema.

Ayen aliongezea, "Sarakasi zake na baby mama zilinikera zaidi. Mwanzo hata hakuniambia ana mtoto. Nilimuuliza mara kadhaa, tukiwa kwa shoo tulikuwa tunazungumza. Nilimuuliza ikiwa ana mke na watoto akasema hapana, eti angali mdogo kuwa na familia. Nilishtuka kuona baby mama akizungumza kuhusu baba asiyewajibika. Aliniomba msamaha huku akidai kuwa alikuwa anajipanga kuniambia"

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke