Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Boeing kuwalipa fidia walipoteza ndugu zao kwenye ajali Ethiopia

Boeing Compenseert Slachtoffers Crash 737 Max Van Ethiopian Boeing kuwalipa fidia walipoteza ndugu zao kwenye ajali Ethiopia

Thu, 11 Nov 2021 Chanzo: BBC

Boeing imefikia makubalano na familia za watu waliopoteza wapendwa wao 157 katika ajali ya ndege ya Ethiopia 737 Max iliyopata ajali mwaka 2019.

Watengenezaji wa ndege wamekubali kuwajibika kutokea kwa vifo hivyo kwa mujibu wa mahakama huko Chicago.

Hivyo familia zilizopoteza ndugu zao hazitatafuta fidia za kile walichopoteza kutoka kwa kampuni.

Mawakili wa familia zilizoathirika bado wamesesema Boeing bado itawajibishwa "kikamilifu", wakikaribisha makubaliano hayo kama hatua muhimu.

Hisa za Boeing zilishuka 1% hadi $218.50 kufuatia habari ile.

Makubaliano yanatoa fursa kwa familia zilizo nje ya Marekani , kama vile Ethiopia na Kenya, kudai fidia kupitia mahakama ya Marekani kuliko kwenye mataifa yao , jambo ambalo litakuwa gumu na matokeo ya malipo kuwa kidogo.

Mark Pegram kutoka Uingereza ambaye mtoto wake alikuwa mhanga wa ajali hiyo amesema: "Jambo muhimu kwao ni Boeing kukiri kuhusika na kuanguka kwa ndege hiyo na sio kuweka lawama kwa marubani wa Ethiopian Airlines ... tulitaka wajisalimishe."

Mama yake Sam Debbie aliiambia BBC: "Tunachoangalia kukifanyia katika fidia yoyote itakayotolewa ni kuanzisha shirika la kusaidia wahitaji kwa jina la Sam. Na hicho ndicho Sam angetaka tufanye."

Wakati wa ajali hiyo ya 737 Max, soko la ndege ya Boeing lilikuwa juu.

Lakini ajali mbili mbaya zilizotokea ndani ya miezi mitano - ya ndege ya Ethiopia iliyotokea Addis Ababa na kabla ya hapo ajali ya ndege ya Lion Air iliyoanguka baharini karibu na Indonesia - iliashiria kuwa na hitilafu kubwa kwenye ndege.

Ndege hizo zilizuiwa kwa muda wa miezi 20, huku uchunguzi ukiendelea, lakini zimeruhusiwa kurejea kazini baada ya kampuni hiyo kufanya mabadiliko makubwa kwenye programu na mafunzo yao.

Chanzo: BBC