Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bobrisky, jamaa aliyejibadilisha kuwa mwanamke ataja sababu

Ee6debfa3186a30b Bobrisky, jamaa aliyejibadilisha kuwa mwanamke ataja sababu

Thu, 30 Sep 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Bobrisky, ambaye alizaliwa mwanamume, alijibadilisha kuwa mwanamkeAlisema wanawake wameshindwa kutumia vizuri kile Mungu amewapa kujitajirishaMnigeria huyo alisisitiza kuwa anataka kujisimamia mwenyewe akitumia alichonacho kupata anachotaka bila kujali wanaomsemaAlifichua kuwa kabla ya kubadilisha jinsia, alikuwa maskini na hakuna aliyeshughulika naye kando na mama yake pekeeIdris Okuneye, ambaye anafahamika kwa wengi kama Bobrisky ni mmoja wa watu maarufu sana nchini Nigeria.

Bobrisky, ambaye alizaliwa mwanamume na kujibadilisha kuwa mwanamke, alisema wanawake wameshindwa kutumia vizuri kile Mungu amewapa.

"Kwa sababu kuwa mwanamke kwa sasa imefungua fursa nyingi. Wanawake hawajui kwa namna gani wana nguvu, wengi wao hawajui kutumia vipaji vyao kama wanawake," alisema Bobrisky katika mahojiano na runinga ya Chude.

Mnigeria huyo alisisitiza kuwa anataka kujisimamia mwenyewe akitumia alichonacho kupata anachotaka bila kujali wanaomsema.

Kulingana na celeb huyo, kabla ya kubadilisha jinsia, alikuwa maskini na hakuna aliyeshughulika naye kando na mama yake pekee.

Lakini alichoshwa na hali hiyo na kutaka kuwa mtu anayejisimamia mwenyewe.



Read also

Mbunge Kanini Kega Azomewa Baada ya Kutetea Bei Ghali ya Mafuta

"Mama yangu ni mtu pekee aliyenipenda sana na kuniunga mkono wakati kila mmoja alikuwa akinikataa.Pesa ni kila kitu. Kama unasema pesa sio kila kitu, unajidanganya mwenyewe. Unahitaji kuwa na hadhi fulani, ikiwemo pesa," aliongezea.

Madai ya kujibadilisha kuwa mwanamkeMnamo Julai 8, 2021, Bobrisky alianika mwili wake mitandaoni kuonyesha muonekano wake mpya baada ya kufanyiwa upasuaji wa kubadilika kuwa mwanamke.

Bobrisky alianza kugonga vichwa vya habari mnamo Mei 2019, alipojitokeza hadharani akitaka atambulike kama mwanamke na wala si mwanamume.

Hata hivyo, uamuzi wake ulipokelewa na hisi mseto mitandoani huku baadhi wakimdhihaki na wengine wakidai ana uhuru na uamuzi wake unatakiwa kulindwa.

Kulinga na ripoti ya Google mwaka 2016, Bobrisky ndiye anaongoza kama mtu aliyesomwa na kutafutwa sana kupitia Google nchini Nigeria.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.



Read also

Migori: Vijana na Kina Mama Waonjeshwa Mamilioni ya DP Ruto
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke