Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bilionea Mamelodi njia nyeupe Urais Caf

Caf Pic Data Bilionea Mamelodi njia nyeupe Urais Caf

Sat, 6 Mar 2021 Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz

Njia imeanza kuwa nyeupe kwa Mmiliki wa Mamelodi Sundowns, Patrice Motsepe kuwa Rais mpya wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (Caf) baada janausiku ya wagombea wawili wa nafasi hiyo Jacques Anouma na Augustin Senghor kutangaza kujiengua katika kinyang'anyiro hicho.

Senghor ambaye ni Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Senegal na Anouma kutoka Ivory Coast aliyewahi kuwa Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya Shirikisho la Mpira wa Miguu Duniani (FIFA) walitangazwa kujitoa katika kile kinachodaiwa kumuunga mkono Motsepe.

Mpango wa Senghor na Anouma kujitoa unadaiwa kusukwa huko Morocco, wiki iliyopita ukiratibiwa na Rais wa FIFA, Gianni Infantino ambaye anadaiwa anamuunga mkono waziwazi Motsepe katika uchaguzi huo unaotarajiwa kufanyika Rabat, Morocco, Machi 12 mwaka huu.

"baada ya mapitio kadhaa na ushauri, nimeamua kujiondoa katika ugombea wa uchaguzi wa nafasi ya Urais ya Caf," alisema Anouma wakati alipotangaza uamuzi wake kupitia kituo cha luninga cha taifa cha Ivory Coast.

Kwa upande wake, Senghor alisema ameamua kuchukua uamuzi huo kwa maslahi mapana ya mchezo wa mpira wa miguu barani Afrika.

"Kujiondoa kwangu katika ugombea wa Urais wa Caf kwa faida ya mgombea mwingine hakuwezi kukubalika na wote kwa sababu mbalimbali. Ninalifahamu hilo lakini naamini ni uamuzi mzuri, uamuzi sahihi," alisema Senghor katika taarifa yake.

Chanzo: www.mwanaspoti.co.tz