Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Bibi harusi agoma kumbusu mume wake harusini

9b2f063970bb08b5 Bibi harusi agoma kumbusu mume wake harusini

Tue, 10 Aug 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Hii ni licha ya bwana harusi kujaribu mara kadhaa kupewa busu lakini alinyimwaKatika video hiyo iliyochapishwa kwenye mtandao wa Instagram, wawili hao ambao wanaonekana kuwa katika mapokezi ya harusiBwana harusi anaonyeshwa akimsongea mahabubu wake akitaka kumpiga busu lakini bibi harusi aligeuza uso wake na kuwaacha wageni wameduwaaVideo inazagaa kwenye mitandao ya kijamii ikimuonyesha bibi harusi akikataa kumupa busu bwana harusi wakati wa hafla yao ya harusi.

Hii ni licha ya bwana harusi kujaribu mara kadhaa kupewa busu lakini alinyimwa.

Katika video hiyo iliyochapishwa kwenye mtandao wa Instagram na yabaleft tv, wawili hao ambao wanaonekana kuwa katika mapokezi ya harusi.

Bwana harusi anaonyeshwa akimsongea mahabubu wake akitaka kumpiga busu lakini bibi harusi aligeuza uso wake na kuwaacha wageni wameduwaa.

Baada ya majaribio kadhaa bila kufua dafu, bwana harusi alifaulu kuguzanisha mdomo wake na mke wake mpya.

Tazama video hiyo hapa

Hata hivyo, huenda bibi harusi huyo alikuwa mwoga na hivyo hakutaka kumbusu bwana harusi hadharani. Hii ni kutokana na video hiyo ambapo anaonyesha tabasamu dhaifu dhahiri kwamba hakuwa na raha.



Wanamtandao walisema nini?Video hiyo ilizua hisia mseto mtandaoni huku wanamtandao wakioa hisio tofauti kuhusu tukio hilo wengine wakihoji kuwa huenda mrembo huyo alilazimishwa.

Hii hapa maoni yao

Yetunde Bakare aliandika:“Anaonekana alilazimishwa na hivyo hakutaka kujidanganya"

egbon_seniorboyy alisema “Hapana ni muoga ama alikuwa anaogopa harufu mbaya ya mdomo"

phinemandy aliandika, “Ex wake yuko hapo"

Mama ahepa na mahari ya binti yakeKatika tukio tofuati la humu nchini, mama mmoja kutoka Tana River aliwaacha mashemeji zake wakiwa wameduwaa baada ya kuhepa na KSh 170,000 za mahari ya bintiye.

Ann Maweni aliwaalika wazee kutoka upande wa marehemu mumewe katika hafla ambapo mpenzi wa bintiye alikuwa amefika kulipa mahari.

Kulingana na Daily Nation, Maweni aliwapakulia chakula wageni wake na wazee wakati wa sherehe hiyo kisha muda mfupi baadaye akatoweka na hela alizopewa akihofia kuandamwa na wazee hao.

Kulingana na dadake Veronica Meilu, mama huyo baadaye alimtumia ujumbe mfupi kumwambia afunge sherehe hiyo baada ya kutoa ujumbe wa shukrani.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke