Serikali ya nchini humo kwa muda mrefu imekuwa ikijitahidi kukuza thamani ya pesa yake ambayo imeporomoka katika soko la dunia tangu mwaka 2009 .
Kuporomoka kwa thamani ya pesa nchini humo kumechochea mfumuko mkubwa bei za bidhaa hali ambayo imepelekea Benki hiyo kuanzisha noti mpya mwa 2016.
Benki hiyo kupitia kitengo chake cha ujasusi (FIU) kimewabaini watu 30 wanaotumia vibaya mitandao ya kijamii na huduma za simu kwa kujiingizia pesa kinyume cha taratibu sambamba na kutakatisha fedha.
Kitengo hicho kimeziagiza Benki zote nchini humo kuzifunga akaunti za watuhumiwa hao ambao wanashutumiwa kufanya shughuli hizo kwa zaidi ya mikaa miwili sasa