Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Babu Owino afichua amekuwa akitafuna cocaine na heroin, asema amebadilika sasa

24e19edd2e4e1169 Babu Owino afichua amekuwa akitafuna cocaine na heroin, asema amebadilika sasa

Thu, 17 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Babu Owino alijipatia umaarufu sana kwa kuwa mwenye sarakasi nyingi wakati wa uongozi wake chuoniKando na mifuko mizito alikuwa ni mtu mwenye uzushi mwingi na hivyo kujipata kwenye utata na serikaliAkiongea na bloga Alai alifichua amekuwa akitafuna cocaine na heroin na hivyo kuchukua maamuzi ambayo si sawaWakati wa uchaguzi wa 2017 alikuwa mmoja wa wandani wa Raila Odinga waliomshambulia Uhuru Kenyatta vikaliMbunge machachari wa Embakasi Mashariki Paul Ongili maarufu kama Babu Owino amekiri kutumia dawa za kulebya maishani.

Akiongea kwenye mahojiano na mwanablogu Robert Alai, Babu alisema alikuwa mraibu wa dawa hizo ambazo zilimfanya kufanya maamuzi mabaya.

Babu anajulikana kwa kuchemka dhidi ya wapinzani wake na wakati wa kampeni za 2017 alipata umaarufu kwa kumchemkia Rais Uhuru Kenyatta.

"Nimewahi kutumia dawa za kulevya kama vile heroin, cocaine na kunywa kila aiana ya vileo. Lakini hilo lilikuwa katika maisha yangu yaliyopita," alisema mbunge huyo.

Alionya kuwa huenda baadhi ya mambo aliyoyafanya yalichochewa na atahri za kulewa kutokana na dawa hizo.

"Nakubali kuwa ukitumia dawa hizo, unaweza kufanya maamuzi mabaya. Hakuna kitu ambacho dawa hizi hukusaidia nacho mwilini," alimwambia Alai wakati wa mahojiano hayo.

Madawa hayo yenye athari kali huwa ni biashara kuu ya vigogo humu nchini na juhudi za serikali kupiga vita ulanguzi zimekuwa bila matunda.



Kwa Babu Owino, vitendo kama kuzua uzushi katika kituo cha polisi au kutoa misimamo mikali alipokuwa kiongozi wa wanafunzi katika chuo kikuu cha Nairobi ilikuwa jambo la kawaida.

Amekuwa akitaka kuchukua mwanzo mpya maishani mwake wakati mmoja alkisema mkewe alikuwa akimuongoza katika kubadilisha mkondo wa maisha yake.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama habari za TUKO hapa
Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke