Afrika

Habari

Burudani

Michezo

Biashara

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Babake Diamond asema hana haja ya kubebwa kwenye gari lake la Rolls Royce

0857ac42d90aa8fd Babake Diamond asema hana haja ya kubebwa kwenye gari lake la Rolls Royce

Mon, 19 Jul 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Babake Diamond Platinumz amesema hana haja ya kuonja utamu wa gari la aina ya Rolls royce la mwanawe ambalo amelinunua hivi maajuziKulingana na Mzee Abdul, anachokisubiri ni kubebwa ndani ya jeneza lake ambalo anaamini litabebwa na wengi ama liwekwe kwenye gariMzee Abdul alisema ameona mengi katika maisha yake na kilichosalia sasa kifo Babake staa wa Bongo Diamond Platinumz Mzee Abdul amesema hana haja ya kubebwa kwenye gari la mwanawe la kifahari aina ya Rolls Royce ambalo alinunua hivi maajuzi.

Habari Nyingine: Crisis Meeting: Jubilee Kukutana Jumatano Kujadili Kichapo cha Kiambaa

Mzee abdul alisema ameona mengi katika maisha yake na anachosubiri kwa sasa ni kubebwa kwenye jeneza lake tu.

Akiwa kwenye mahojiano na bloga wa Tanzania, Mzee Abdul aliulizwa sababu ya kutotaka kuonja utamu wa gari la mwanawe ambalo aina yake haimilikiwi na wengi nchini humo na alikuwa na haya yakusema,



Read also

Mimi ni Mke wa Mtu Tafadhali Msipige Simu Baada ya Saa za Kazi, Chifu awaonya Wakaaji

" Kama kuna kitu ambacho sijakitumia ni jeneza, nimeona mengi katika maisha yangu, nasubiri tu kubebwa kwenye jeneza kakangu," Alisema Abdul kisha kumalizia na maombi.

Kulingana na matamshi haya, ni wazi kwamba Mzee Abdul ameshakata tamaa maishani na anachosubiri sasa ni kuiondokea dunia.

Awali, Mzee Abdul alisema kwamba sio lazima Diamond ahudhurie mazishi yake akifa kwa sababu atazikwa na watu wengine wanaomthamini.

" Sio lazima nikifa aje kunizika kwa sababu mimi ni mtu wa watu, nitazikwa na watu wengine. Huenda wakati nitakaokufa atakuwa ameondoka nchini au awe ameshikika kwenye shughuli zingine," Abdul alisema.

Diamond amekuwa akiwahakishia mashabiki wake kwamba gari lake la Rolls Royce lilikuwa njiani na kwa kweli alilipokea Jumanne, Julai 14 nyumbani kwake.

Kupitia picha kadhaa alizopakia kwenye mitandao, Diamond alionekana ameketi kwenye gari hilo, kando yake kulikuwa na magari mengine matano ya kifahari anayomiliki.



Read also

Mimi Siwezi Kuolewa na Mwanamume Maskini, Asema Mwimbaji Justina Syokau

Diamond amethibitisha utajiri wake kwani gari hilo linamilikiwa na wachache, mwanamuziki Davido ni mmoja wao.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Tazama Video Kemkem za Kusisimua Kutoka hapa TUKO.co.ke.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke