Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Video ya Magufuli akisema aliandamwa na maadui wengi yazuka:

80549b3d13f3fe0c Video ya Magufuli akisema aliandamwa na maadui wengi yazuka:

Wed, 24 Mar 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais John Pombe Magufuli alifichua kwamba alikuwa amelishwa sumu na mawaziri 'wenye wivu' ambao walitumikia chini ya Rais wa zamani Benjamin Mkapa

- Hayati marehemu kiongozi huyo wa Tanzania alisema maafisa wengine wa ngazi za juu walianza kupanga njama dhidi yake wakati alipokuwa akiongoza Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu

- Katika video nyingine iliyoibuka mitandaoni, Magufuli pia alisema alikuwa na maadui wengi, hata kutoka mataifa ya nje, baada ya kusimamisha kampuni za kimataifa kuchimba dhahabu

Video ya hisia kali ya rais wa zamani wa Tanzania, Hayati Dkt. John Pombe Magufuli, akifunguka na kusema alikuwa na maadui wengi ambao walimtakia kifo imeibuka tena wiki moja baada ya kifo chake kilichotangazwa wiki jana.

Kwenye kipande cha video ambacho TUKO.co.ke imekitizama, kiongozi wa zamani wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) alifunguka kuhusu kulishwa sumu na mawaziri "wenye wivu" ambao walitumikia chini ya Rais wa Marehemu Benjamin Mkapa.

“Nakumbuka nilifanya kazi na Rais Benjamin Mkapa. Mara moja aliniita kama msaidizi wake wa kwanza kutokana na kazi nzuri niliyokuwa nikifanya katika Wizara ya Maendeleo ya Miundombinu. Siwezi kusahau tukio hilo kwa sababu, licha ya hisia nzuri za Mkapa, iliniingiza matatani,” Magufuli alisema.

Hotuba Nzito ya Rais Samia Suluhu Wakati wa Kumuaga Hayati Magufuli Jijini Dodoma

Magufuli, ambaye alipewa jina la Bulldozer wakati wa uwaziri wake kwa sababu ya mtazamo wake wa kutoruhusu uzembe kazini alisema baada ya kupokea sifa kwa utendakazi wake mzuri, maafisa wengine wa ngazi za juu walianza kupanga njama dhidi yake.

“Nilianza kuona dalili kwamba baadhi ya mawaziri wa ngazi za juu serikalini walianza kunichukia. Niliwekewa sumu huko Dodoma na karibu kupoteza maisha. Lakini kwa sababu ya neema ya Mungu, niliepuka kifo. Nilifikiria hata kujiuzulu lakini Mkapa alinishauri niendelee kufanya kazi," alisimulia.

Katika video nyingine iliyoibuka, marehemu kiongozi huyo wa Tanzania pia alisema alikuwa na maadui wengi hata kutoka mataifa ya nje baada ya kusimamisha kampuni za kimataifa kuchimba dhahabu nchini kwa manufaa ya wenyeji.

"Dhahabu yetu inachimbwa na kusafirishwa nje ya nchi hata kama raia wetu wanakabiliwa na umaskini. Wenyeji wanafukuzwa kutoka maeneo yenye utajiri mwingi wa madini ili wao (wageni) waweze kuchimba na kufaidika peke yao. Nilipoingia madarakani, niliacha hii na kuwauliza waje kwenye meza ya mazungumzo. Hii ilinipatia maadui wengi," Magufuli alisema.

Kifo na maziko ya MagufuliKifo cha Magufuli kilitangazwa Jumatano, Machi 17, na ilisemekana kilitokana na matatizo ya moyo, ambayo alikuwa akipambana nayo kwa miaka mingi.

Baada ya kifo chake, Makamu wa Rais Samia Suluhu aliapishwa ofisini na akaandika historia ya kuwa kiongozi wa kwanza mwanamke katika nchi hiyo ya Afrika Mashariki kuwa rais.

Kiongozi huyo wa CCM atazikwa nyumbani kwake Chato, mkoani Geita Ijumaa, Machi 26.

Read ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Francis M Silva ni Mkuu wa Kitengo cha Kiswahili katika TUKO.co.ke. mwenye tajriba ya miaka mingi katika taaluma ya uwanahabari hasa uhariri - Radio, TV na Mitandaoni. Yeye ni zao la Chuo Anuwai cha Mawasiliano (KIMC). Amefanya kazi katika Radio Umoja, Good News Broadcasting System (GBS TV) na Idara ya Michezo ya Runinga ya Shirika la Utangazaji nchini KBC hadi leo. Hutumia tajriba yake kubwa katika kufanya iwe bora zaidi ya ilivyokuwa.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke