Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Uhuru Kenyatta ahuduhuria hafla ya kumuapisha Rais Yoweri Museveni

2d319908aeca8473 Uhuru Kenyatta ahuduhuria hafla ya kumuapisha Rais Yoweri Museveni

Thu, 13 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Uhuru, ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, aliandamana na Mawaziri Raychelle Omamo, Peter Munya na James Macharia

- Marais Felix Tshisekedi wa Congo, Alpha Conde wa Guinea , Salva Kiir Mayardit wa Sudan Kusinimiongoni mwa wengineo walihudhuria sherehe hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Kololo Independence Grounds mjini Kampala

- Museveni alichaguliwa tena kuwa Rais wa Uganda mnamo Januari 17, 2021 kwenye uchaguzi uliokuwa na ushindani mkali kutoka kwa mshindani wake Bobby Wine

Rais Uhuru Kenyatta Jumatano, Mei 12 alijiunga na Marais wa mataifa mengine Barani Afrika katika hafla ya kumuapisha Rais Yoweri Museveni huko Kampala, Uganda.

Uhuru, ambaye sasa ni Mwenyekiti wa Jumuiya ya Afrika Mashariki, aliandamana na Mawaziri Raychelle Omamo (Mambo ya nje), Peter Munya (Kilimo) na James Macharia (Miundombinu).

Marais Felix Tshisekedi (DR Congo), Alpha Conde (Guinea), Salva Kiir Mayardit (Sudan Kusini), Hague Geingob (Namibia) na Nana Akufo Addo (Ghana) walihudhuria sherehe hiyo iliyofanyika kwenye Uwanja wa Kololo Independence Grounds mjini Kampala.

Wengine walikuwa Emmerson Mnangagwa (Zimbabwe), Mohamed Abdullahi Faarmajo (Somalia), Evariste Ndayishimiye (Burundi), Samia Suluhu Hassan (Tanzania), Sahle-Work Zewde (Ethiopia).

Katika hotuba yake ya kuapishwa, Museveni alisema Uganda imepiga hatua kiuchumi hadi katika uzalishaji wa kilimo wakati wa utawala wake.

"Mwaka 1986, Uganda ilikuwa nchi ya uhaba, hakuna sukari, hakuna sabuni, hakuna mafuta ya taa, hakuna nguo, hakuna chumvi, hakuna soda, hakuna bia, hakuna petroli nk. Lakini sasa tunaona mabadiliko ambapo Uganda imekua kwa kiasi kikubwa, ” alisema.

Kiongozi huyo wa Uganda alimshukuru Uhuru na marais wengine kwa kufungua masoko yao kupokea bidhaa kutoka Uganda ikiwa ni pamoja na sukari na mahindi.

Wakati huo huo, Museveni alisuta mamlaka za kigeni ambazo hakuzitaja kwa kukosoa nchi za Kiafrika kuhusiana na utawala akisema baadhi ya mapendekezo yao na ushauri hauna maana ya msingi.

“Inachekesha sana kuona watu wengine wanajaribu kutufunza kuhusu masuala ya demokrasia. Wewe nawe una sifa zipi? Ikiwa unataka kujua tunachofanya kwa njia ya heshima tutakuonyesha, lakini sio kutupa msomo, ” Museveni alishauri.

Museveni alichaguliwa tena kuwa Rais wa Uganda mnamo Januari 17, 2021, huku tuhuma za wizi wa kura zikishamiri uchaguzi huo ambao ulikuwa na ushindani mkali kutoka kwa mpinzani wake mkuu Bobi Wine.

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke