Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Museveni atua Tanzania kwa ziara ya siku moja, alakiwa na Rais Suluhu

F83b109ea903c38b Rais Museveni atua Tanzania kwa ziara ya siku moja, alakiwa na Rais Suluhu

Thu, 20 May 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

Rais Yoweri Museveni ametua nchini Tanzania kwa ajili ya ziara ya kikazi kufuatia mwaliko wa Rais wa nchi hiyo Mheshima Rais Samia Suluhu.

TUKO.co.ke imefahamishwa kwamba Rais Museveni alilakiwa na Rais Suluhu na wakafulululiza hadi katika ikulu ya Dar es Salaam ambapo wanafanya mkutano wao.

Agenda kuu ya mkutano huo ni kwa marais hao kushuhudia utiaji saini wa mikataba ya utelekeza wa mradi wa bomba la mafuta kutoka Uganda hadi Bandari ya Tanga nchini Tanzania

Mkutano huu unajiri mwezi mmoja baada ya Rais Suluhu pia kumtembelea Rais Museveni kujadili kuhusu mradi huo.

Imekisiwa kwamba bomba la mafuta lenye thamani ya dola za Kimarekani bilioni 4.1 linatarajiwa kuunda ajira kwa vijana zaidi ya 15, 000.

Mpango wa utekelezaji wa bomba hilo ulianza kuzungumziwa kati ya mataifa haya mawili mwaka wa 2017 wakati wa utawala wa Hayati Rais John Pombe Magufuli.

Rais Suluhu alifanya ziara yake ya kwanza nchini Uganda majuma kadhaa baada ya kuchuku hatamu za uongozi kufuatia kifo cha aliyekuwa mtangulizi wake Rais Magufuli.

Itakumbukwa kwamba Rais Suluhu hakuwa akivalia barakoa lakini pindi alipotua nchin Uganda, picha zake zilienezwa mitandao akiwa amevalia.

Akiwa nchin mwake, inaonekana Rais huyo alikuwa akiendeleza uliokuwa msimamo wa Hayati Magufuli kwamba hakuna ugonjwa wa corna nchini humo na hivyo hakuaona hoja ya raia kuvalia barakoa.

Hata hivyo, inaonekana Rais Suluhu amechukua mkondo mpya kwani katika ziara yake ya hivi punde nchini Kenya, alionekana akiwa amevalia barakoa na kuzingatia masharti ya covid-19.

Tayari ameagiza jopokazi liundwe nchini Tanzania ili kutathmini hali ya coronavirus nchini humo na kutoa ushauri kwa serikali.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke