Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Rais Museveni afunga makanisa, shule kwa siku 42 kuzuia msambao wa COVID-19

203c7d3f08b5c1eb Rais Museveni afunga makanisa, shule kwa siku 42 kuzuia msambao wa COVID-19

Mon, 7 Jun 2021 Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke

- Rais wa Uganda Yoweri Museveni siku ya Jumapili, Juni 6, alitoa masharti mapya ya kuzuia kuenea kwa COVID-19

- Kulingana na Museveni, hali ya sasa ya COVID-19 nchini humo ni ya kutisha akiongezea kuwa idadi ya vifo imepanda maradufu ikilinganishwa na wimbi la kwanza

Rais wa Uganda Yoweri Museveni ameamuru kufungwa kwa shule makanisa na misikiti kwa siku 42 ili kudhibiti kuenea kwa COVID-19 katika taifa hilo la Afrika Mashariki.

Kulingana na rais huyo, janga la COVID-19 limeathir pakubwa taifa hilo huku visa 825 vipya vya maambukizi vikiripotiwa kila siku.

Akizungumza Jumapili, Juni 6, Museveni alisema masharti hayo mapya yataanza kutekelezwa Jumatatu Juni 7.

"Katika wimbi hili maambukizi na vifo vya wagonjwa wa COVID-19 imepanda kuliko ilivyoshuhudiwa wakati wa wimbi la kwanza la janga," alisema.

Kiongozi huyo wa taifa pia alipiga marufuku magari ya uchukuzi wa umma kusari kutoka kwa mkoa mmoja hadi nyingine kunzia Juni 10.

“Hii ni kuwaruhusu watato wetu kusafiri kutoka shuleni hadi manyumbani kwao. Tunapiga marufuku mikutano ya hadhara kwa siku 42,” Museveni aliongezea.

Alisema serikali yake imejitolea kuwachanja watu 21.9 milioni nchini humo ikianza na watu walioko kwenye mstari wa mbele 4.8 milioni.

Kulingana na Wizara ya Afya ya Uganda, kuanzia Januari hadi Aprili, makali ya maambukizi yalipungua kwa 3%, lakini yalianza kupanda tena Mei ikifikia 18% Juni 2.

Itakumbukwa kuwa Uganda iliweka masharti makali ya kutoka nje janga hilo lilipotua nchini humo.

TUKO.co.ke iliipotia kuwa Uganda ilithibitisha kisa cha aina mpya COVID-19 ya India.

Wizara ya Afya ilithibitisha katika taarifa mtandaoni kufuatia matokeo yaliyotolewa Alhamisi, Aprili 29.

READ ENGLISH VERSION

Je, unayo taarifa ya kusisimua ambayo ungependa tuichapishe? Tafadhali, wasiliana nasi kupitia [email protected] au WhatsaApp: 0732482690.

Chanzo: kiswahili.tuko.co.ke