Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Naomba nikabidhiwe jeshi langu - Mtoto wa Museveni

Museveni Muhoozi 89.jpeg Naomba nikabidhiwe jeshi langu - Mtoto wa Museveni

Sat, 2 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Mtoto Rais wa Uganda Yoweri Museveni, Jenerali Muhoozi Kainerugaba amezua gumzo mitandaoni kwa kudai Jeshi la Uganda ni lake.

Kwenye ukurasa wake wa Twitter (X), Jenerali Muhoozi alisema jeshi la Uganda ni lake na linapaswa kukabidhiwa kwake.

Huku akinukuu hisia za Kanali Jet Mwebaze kuwa “Wafu pekee ndio wameona mwisho wa vita” Muhoozi alisema kwa kuwa bahati inawapendelea wana wa Mungu, hivyo basi atapendelewa kuwa rais wa Uganda siku moja.

“UPDF bado ni Jeshi Langu. Afande Mzee nataka jeshi langu lirudi! Bahati inawapendelea wana wa Mungu! Nitakuwa Rais wa Uganda siku moja!,” Muhoozi aliandika kwenye akaunti yake ya Twitter.

Aliendelea kuandika, “Nitakufanyia jina kuu miongoni mwa wakuu duniani… Hili ndilo neno la Bwana wa Majeshi. Nilikuchukua kutoka malishoni na kutoka kuwafuata ng’ombe kuwa Mkuu juu ya watu wangu Uganda. Nimekuwa pamoja nawe popote ulipoenda, na nimewaangamiza adui zako wote katika njia yake,” alijigeuza.

Mwezi uliopita Muhoozi, anayejulikana kama Tweeting General, alisema anataka kuwa rais wa Uganda kwa heshima ya mama yake Janet Museveni.

Katika mfululizo wa ‘milipuko’ ya Twitter kuhusu kuchukua madaraka baada ya babake, ambayo pia iliweka upande wa upinzani kwenye vichwa vya habari, Kainerugaba alisema kuwa akiwa rais wa Uganda ndiyo njia bora ya kumthamini mama yake.

“Njia pekee ninayoweza kumlipa mama yangu mkubwa ni kwa kuwa Rais wa Uganda! Na nitafanya hivyo!” alisema. Uganda itapiga kura mwaka 2026. Museveni ameiongoza nchi hiyo tangu alipoingia madarakani mwaka 1986.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live