Wagosi wa Kaya, Timu ya Coastal Union imewachapa wenyeji, KMC 2-3 Uwanja wa Azam Complex, Chamazi, nje kidogo ya Jiji la Dar es Salaam siku ya Jumatatu.
Mabao ya Coastal Union yamefungwa na Abdul Hamisi kwa penalti dakika ya 22, William Kisingi dakika ya 82 na Rashid Chambo dakika ya 90 na ushei, wakati ya KMC yamefungwa na Emmanuel Mvuyekure dakika ya 40 na Kenny Ally dakika ya 47.
Huu ni ushindi wa Kwanza kwa Coastal tangu walipomtimua Kocha wao Mmarekani Melis Medo kutokana na mfululizo wa matokeo mabovu.
Tanzania Web inakuletea video iliyokusanya matukio yote muhimu katika mchezo huo;