Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Museveni: Serikali haitafanya chochote kudhibiti mfumuko wa bei

Museveni Jn.jpeg Yoweri Museveni, Rais wa Uganda

Mon, 23 May 2022 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Uganda Yoweri Museveni amesema serikali haitaingilia kati hali ya sasa ya kiuchumi na kupanda kwa gharama ya maishi nchini humo .

Bei za bidhaa za mafuta, i mali ghafi inayoagizwa kutoka nje ya nchi, pamoja na chakula, zimekuwa zikipanda katika miezi michache iliyopita, mzozo ambao unashuhudiwa kute duniani kufuatia vita vya vinavyoendelea nchini Ukraine.

Mfumko wa bei nchini Uganda umefikia asilimia 4.9, kiwango cha juu zaidi kuwahi kushuhudiwa tangu mwaka 2017.

Katika hotuba yake kwa taifa kupitia televisheni usiku wa Jumapili, Museveni alisema ruzuku ya serikali au kuondolewa kwa ushuri wa bidhaa zinazoagizwa nje ya nchi kutaporomosha uchumi..

Kutumia kwa akiba ya kitaifa kwa ununuzi wa bidhaa hizo za bei ghali kutakuw ana athari kubwa, rais aliongeza.

Akiba ya sarafu ya kigeni nchini Uganda kwa sasa ni zaidi ya bilioni nne

Bw. Museveni alisema nchi inatakiwa kutumia bidhaa za kuagizwa kutoka ambazo inaweza kumudu pekee

Pia aliwashauri wananchi kubadilisha ngano ya bei ghali badala ya vyakula vinavyopatikana nchini kama vile mtama, mahindi, ndizi mbichi na mihogo..

Sehemu kubwa ya Uganda ina uwezo wa kuzalisha vyakula kwa wingi, na familia nyingi zinategemea kilimo cha kujikimu.

Kati ya 2020 na 2021, kilimo kilichangia takriban asilimia 23.7 ya Pato la Taifa la nchi. Lakini hata bei za vyakula vinavyozalishwa nchini zimekuwa zikipanda, hasa mijini, kutokana na gharama za usafirishaji.

Raia wa Uganda wanalazimika kununua kiasi kidogo cha vitu vya msingi au kuegesha magari yao ili kukabiliana na mzozo huo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live