Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Mauaji watu 560 yamuibua Rais Museveni

Adf Dede Mauaji watu 560 yamuibua Rais Museveni

Sat, 9 Sep 2023 Chanzo: www.tanzaniaweb.live

Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, amearifu kuwa wanajeshi wake wamewaua zaidi ya wanachama 560 wa kundi la waasi la DF linaloshirikiana na Islamic State, tangu walipoanzisha operesheni dhidi yao Desemba 2021.

Kundi linaloipinga Kampala la Allied Democratic Forces – ADF, linaendesha shughuli zake katika misitu ya mashariki mwa Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo – DRC, ambako linafanya mashambulizi ndani ya Congo na Uganda.

Baada ya kupata kibali toka DRC, Wanajeshi wa Uganda walianzisha operesheni dhidi ya ADF wakitaka kuharibu kambi zao na kuua au kuwakamata wapiganaji wa kundi hilo.

Chanzo: www.tanzaniaweb.live