Klabu ya Olympique de Marseille ya nchini Ufaransa imefanikiwa kuifunga timu ya RB Leipzig kwa jumla ya mabao 5 – 2 usiku wa kumakia leo kwenye dimba la Stade Velodrome na kujikatia tiketi ya kutinga hatua ya nusu fainali ya michuano ya Europa League.
Marseille ambayo imetinga hatua hiyo kwa kupitia wachezaji wake, S Ilsanker aliyefunga dakika ya 6,B Sarr (9),F Thauvin (38),D Payet (60) na H Sakai aliyetupia (90+4) huku RB Leipzig wakipata ya kufutia machozi kupitia kwa wachezaji wake Bruma (2), na J Augustin (55). hata hivyo vijana hao wa Ufaransa wanapita kwa jumla ya mabao 5 – 3 dhidi ya RB Leipzig baada ya kuwa na bao moja kwenye mchezo wao wa kwanza.
Picha za matukio uwanjani wakati wa mchezo wa Marseille ya nchini Ufaransa dhidi ya timu ya RB Leipzig