Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Marekani inaendelea na juhudi za kumaliza mgogoro wa Gaza

Marekani Inaendelea Na Juhudi Za Kumaliza Mgogoro Wa Gaza.png Marekani inaendelea na juhudi za kumaliza mgogoro wa Gaza

Tue, 17 Sep 2024 Chanzo: Voa

Marekani inashirikiana kikamilifu na washirika wakuu wa kikanda, hasa Misri na Qatar, kuwasilisha pendekezo lililorekebishwa la kusitisha mapigano Gaza.

Wakati ratiba ya pendekezo hilo inayotarajiwa kuchukuwa wiki kadhaa, bado haijatolewa, msemaji wa Wizara ya Mambo ya Nje ya Marekani, Matthew Miller amewaambia wanahabari Jumatatu kwamba Washington inafanya kazi kwa haraka kuhakikisha pendekezo hilo linaleta makubaliano ya mwisho kati ya Israel na Hamas.

Mapema Jumatatu, Waziri wa Mambo ya Nje wa Marekani, Antony Blinken alikutana na Yair Lapid, kiongozi wa upinzani wa Israel na waziri mkuu wa zamani.

Baada ya mkutano huo katika Wizara ya Mambo ya Nje, Lapid aliwaambia wanahabari kwamba Israel inataka makubaliano ya mateka na kusitisha vita, akisisitiza hakuna mchakato wa kisiasa au misukosuko inayopaswa kuathiri mpango huo.

Chanzo: Voa