Thu, 5 Jan 2023
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
BAO la winga Dickson Isaac Ambundo limeipa Yanga SC ushindi wa 1-0 dhidi ya wenyeji, KMKM katika mchezo wa Kundi B michuano ya Kombe la Mapinduzi jana usiku Uwanja wa Amaan, Zanzibar.
Ambundo alifunga goli hilo dakika ya 90 na ushei sekunde chache kabla ya kipyenga cha mwisho na sasa Yanga watalazimika kushinda mechi ya mwisho dhidi ya Singida Big Stars keshokutwa ambayo ihitaji taji sare tu ili kwenda Nusu Fainali.
Tanzaniaweb inakusogezea matukio yote muhimu yaliyojitokeza katika mchezo huo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live