Michezo

Habari

Burudani

Biashara

Afrika

Live Radio

Nchi

Kijamii

Lifestyle

SIL

Magufuli ateua viongozi watano, yumo bosi wa NIMR

77413 MAGU+PIC

Fri, 27 Sep 2019 Chanzo: mwananchi.co.tz

Dar es Salaam. Rais wa Tanzania, John Pombe Magufuli leo Alhamisi Septemba 26, 2019 amefanya uteuzi wa viongozi mbalimbali.

Kwanza, Rais Magufuli amemteua Profesa Blasius Nyichomba kuwa Mwenyekiti wa Baraza la Uongozi wa Chuo cha Taifa cha Usafirishaji (NIT). Profesa  Nyichomba ni Profesa Mshiriki wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Pili, Rais Magufuli amemteua Dk Rosemarie Mwaipopo kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Uendeshaji ya Taasisi ya Maendeleo ya Jamii Tengeru. Dk Mwaipopo ni Mhadhiri Mwandamizi wa Chuo Kikuu cha Dar es Salaam (UDSM).

Tatu, Rais Magufuli amemteua Profesa Longinus Rutasitara kuwa Mwenyekiti wa Bodi ya Wakurugenzi wa Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA).

Nne, Rais Magufuli amewateua Rhoda Ngamilanga na Devotha Christopher Kamuzora kuwa Makamu Wenyeviti wa Baraza la Rufani za Kodi.

Tano, Rais Magufuli amemteua Profesa Yunus Mgaya kuwa Mkurugenzi Mkuu wa Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (NIMR). Profes Mgaya anashika wadhifa huo kwa kipindi kingine cha miaka mwili.

Pia Soma

Advertisement

Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu Kiongozi nchini Tanzania, Balozi John Kijazi imeeleza uteuzi wa viongozi hao umeanza leo Septemba 26, 2019.

 

 

Chanzo: mwananchi.co.tz