Kutokana na Kupachika magoli kila leo, Baadhi ya Mashabiki wa Yanga wameamua kumzawadia Mshambuliaji wao Fiston mayele ngo'mbe.
Kwa mara ya kwanza Mayele alizawadiwa Ng'ombe katika mechi dhidi ya Mtibwa Sugar iliyopigwa Manungu Complex Mkoani Morogoro.
Sasa mashabiki wa wekundu wa Msimbazi nao wanatamba kwa kusema kiwango anachokionesha Mchezaji wao Pape Ousmane Sakho anastahili Zawado kubwa zaidi.
Shabiki wa Simba, Maarufu kama Mzaramo ameweka wazi kwamba watampa zawadi kiungo Pape Sakho tena ngamia huku akimwaga tambo baada ya timu hiyo kushinda mabao 2-0 dhidi ya Dodoma Jiji, Uwanja wa Mkapa siku chache zilizopita.