Mon, 25 Apr 2022
Chanzo: www.tanzaniaweb.live
Rais wa Rwanda Paul Kagame amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Uganda Yoweri Museveni mjini Kampala kwaajili ya kuimarisha hali ya usalama nchini Congo.
Mazungumzo hayo yamefanyika April 22, 2022 huku wakilenga katika kuboresha amani na umoja baina ya nchi zote mbili sambamba na kuimarisha ulinzi nchini Congo.
Hata hivyo hatua hiyo ya mazungumzo imekuja mara baada ya kumalizika kwa Mkutano Mkuu wa Wakuu wa nchi za Afrika Mashariki uliofanyika mjini Nairobi nchini Kenya ambao uliagiza kufanyika kwa mazungumzo ya kikanda ili kuimarisha usalama nchini Congo.
Chanzo: www.tanzaniaweb.live